• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kamisaa Makinda azungumzia sensa Dodoma Makulu

Imewekwa tarehe: September 7th, 2021

Na Getruda Shomi, DODOMA

KAMISAA wa Sensa ya Watu na Makazi Anna Makinda amewaasa wananchi wa Kata ya Dodoma Makulu katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kujitokeza kwa wingi siku ya kufanya sensa ya majaribio ya watu na makazi ambayo inayotarajiwa kufanyika kuanzia Septemba 11 hadi 13, 2021 katika Kata hiyo ikiwa ni majaribio ya kupima nyenzo zilizoandaliwa ikiwemo mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) itakayotumika katika zoezi hilo nchi nzima mwakani.

Aliyasema hayo kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa Kata hiyo uliofanyika katika uwanja wa Ofisi ya Mtendaji wa Kata na kuhudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri, Diwani wa Kata hiyo Fadhili Chibago pamoja na Wenyeviti wa Mitaa.

Akiwaeasa wakazi hao kutoa ushirikiano mkubwa kwa mawakala wa sensa ya majaribio na wale watakaofanya sensa rasmi mwaka 2022, Makinda aliwaomba wananchi hao kutoa taarifa sahihi kwa kila swali litakalo ulizwa pasipo kuwa na udanganyifu wowote ili Serikali ipate taarifa sahihi kuhusu watu na makazi, lakini pia sensa ni siri na mawakala hao wameapa kutunza siri.

“Zoezi la sensa ni la siri na litafanyika kwa siri, tunaomba muondoe hofu” alisema Makinda.

Akizungumzia lengo la zoezi la sensa ya watu na makazi, Kamisaa Makinda alisema ni kutambua idadi ya watu nchini, kujua ubora wa nyumba, kiwango cha umaskini na maendeleo, lakini pia nyumba kupewa anuani kwa lengo la kutambua wakazi wa kaya husika.

Alisema idadi ya mikoa iliyotengwa kwa ajili ya sensa ya watu na makazi ya majaribio ni 18, ikiwemo mitano ya Zanzibar na kwa Tanzania Bara ni Mikoa 13.

Awali wakati akimkaribisha Kamisaa Makinda, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri alisisitiza kuwa, sensa ya watu na makazi ni muhimu na kila mwananchi ni haki yake kuhesabiwa ili kutambulika na serikali.

Sensa ya watu na makazi itafanyika rasmi mwaka 2022 ikiwa ni sensa ya sita tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961 na hufanyika kila baada ya miaka kumi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.