• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kampeni ya ‘Sepesha Rushwa Marathoni’ yazinduliwa Dodoma

Imewekwa tarehe: September 19th, 2022

Na. Josephina Kayugwa, DODOMA.
MWENYEKITI wa Mabalozi wa Sauti ya Wapinga Rushwa Mkoa wa Dodoma, Haruna Kitenge, amezindua kampeni ya “Sepesha Rushwa marathon” yenye lengo kujenga uelewa wa jinsi gani ya kupinga rushwa na kuhamasisha sauti za jamii nchini Tanzania.

Kampeni hiyo imezinduliwa katika uwanja wa mpira wa miguu Jamhuri Dodoma ambapo Mwenyekiti huyo amesema vijana ndio Taifa la kesho hivyo wanatakiwa kuelimishwa juu ya madhara ya rushwa kwa sababu rushwa ni adui wa haki.

“Kwa mwaka 2022 mbio hizi zitafanyika Jumapili tarehe 11 Disemba, katika jiji la Dodoma. Mbio hizo zinatarajia kujumuisha washiriki zaidi ya 2,000 kutoka Tanzania nzima, hivyo vijana wahamasike kushiriki ili tuweze kuelimishana kuhusu madhara ya rushwa.

Usajili umeanza rasmi tarehe 16/9/2022 na unafanyika kupitia tovuti yetu ya www.anticorruptionvoices.or.tz au www.eventbrain.com ambapo katika tovuti hizi utakuta ukurasa wa Sepesha Rushwa Marathon na usajili utafanyika kwa awamu tatu kwa gharama tofauti kulingana na awamu yako utakayoamua kujisajili,” alisema Kitenge.

Aidha, alisema kuwa anawaomba wadau na taasisi mbalimbali kuunga mkono ili kuweza kufikisha ujumbe sehemu mbalimbali na kuisaidia Serikali juu ya mapambano dhidi ya rushwa.

Lakini pia alimshukuru Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweli na Serikali nzima ya Jiji la Dodoma kwa kuwaunga mkono katika uzinduzi wa kampeni ya “Sepesha Rushwa Marathoni”.

Kwa upande wake Katibu wa riadha Mkoa wa Dodoma Robert Mabonye, amesema Wilaya zote zijitokeze kushiriki mbio hizi ili kusambaza ujumbe Tanzania nzima.

“…nawashauri watu wote katika kushiriki mbio hizi kwa sababu mazoezi ni afya lakini pia ni kwa lengo la kupambana na Rushwa na kuitokomeza zaidi,” alisema Mabonye.

Katibu wa riadha Mkoa wa Dodoma Robert Mabonye (aliyesimama) alipokuwa akiongea wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya 'Sepesha Rushwa Marathoni' jijini Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.