• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kata 41 jijini Dodoma kunufaika na Milioni 150 za Miradi ya Maendeleo

Imewekwa tarehe: February 5th, 2025

Na. Shahanazi Subeti, DODOMA

Baraza la Madiwani wa Jiji la Dodoma wameipongeza Halmashauri ya Jiji chini ya Mkurugenzi na jopo lake kwa kutenga shilingi bilioni saba kwa ajili ya kumalizia miradi viporo na shilingi milioni 150 kwa kila kata kuanzisha miradi mipya ili kuleta maendeleo kwa wananchi.

Madiwani waliyasema hayo katika mkutano maalum wa kupitia rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe, alisema kuwa Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma inalenga kukamilisha miradi viporo katika jumla ya kata 41 za halmashauri hiyo. “Kwa mwaka huu, Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma inafikia takribani shilingi Bilioni 147 inayolenga kwenda kukamilisha miradi viporo katika kata zetu 41. Miradi yote ambayo haikuisha kwa wakati kutokana na sababu zozote zile. Hivyo, tayari imetengwa kiasi cha shilingi Bilioni saba ili iweze kwenda kukamilisha hivyo viporo” alisema Prof. Mwamfupe.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Kilimani, Neema Mwaluko, alisema Mpango na Bajeti umekuwa ni mzuri sana na umelenga kwenda kuwasaidia wananchi wa kawaida ili kuwanyanyua kiuchumi. “Tukiangalia katika mpango huu na Bajeti, lengo mojawapo ni kumaliza viporo katika kata zetu. Mpango na Bajeti hii umekuwa ni mpango rafiki sana kwa mazingira ya kutoa huduma kwa wananchi wetu. Kwahiyo, naipongeza sana Timu ya Menejimenti ya Jiji ikiongozwa na mkurugenzi na Baraza la Madiwani” alisema Mwaluko.

Nae, Diwani wa Viti Maalum, Anna Mng’ong’o, alimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa bajeti hiyo na kusema kuwa itasaidia kutatua matatizo katika kata na kuleta maendeleo. “Bajeti yetu ipo vizuri sana, bajeti hii imetenga shilingi Billioni 7, kwa ajili ya kumalizia miradi yote viporo katika Kata zetu. Tunaamini kwa Bajeti hii itaenda kujibu na kumaliza matatizo yote, hilo ni jambo la kujivunia sana” alisema Mng’ong’o.

Aidha, Diwani, Wendo Kutusha, alipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kufanya kazi kubwa katika kata kwa kutoa fedha kwa ajili ya maendeleo ya wananchi. “Kutengewa shilingi Milioni 150 kwa kila kata kwa ajili ya miradi ya maendeleo, sisi madiwani tunashukuru na tutahakikisha zinatumika kwa usahihi. Dodoma yetu itabadilika na litakuwa Jiji la mfano” alisema Kutush

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.