• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kata cha Chamwino yadhamilia kutekeleza mkataba wa lishe

Imewekwa tarehe: September 24th, 2023

Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO

KATA ya Chamwino imetakiwa kusimamia utekelezaji wa mkataba wa Lishe kwa mujibu wa maelekezo ya serikali ili kukabiliana na tatizo la utapiamlo katika jamii.

Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Chamwino, Jumanne Ngede aliyekuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe Mtaa wa Mailimbili aliyofanyika katika mtaa wa Mailimbili.

Ngede alisema kuwa ni jambo zuri kwa wataalam na Afisa Mtendaji wa Kata ya Chamwino kusimamia suala la Lishe kutokana na umuhimu wake katika jamii. Alisema kuwa kutokana na umuhimu wake, serikali ilisaini mkataba wa Lishe na makundi mbalimbali ili watekeleze mkataba huo kwa kuhakikisha elimu ya Lishe inatolewa na utekelezaji wa mkataba huo.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege alisema kuwa suala la utekelezaji wa mkataba wa Lishe ni maelekezo ya serikali yanayotakiwa kutekelezwa kwa uzito mkubwa. “Tumeshasaini mkataba wa Lishe, utakumbuka Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alisaini mkataba na wakuu wa mikoa. Wakuu wa mikoa wakasaini na wakuu wa wilaya. Wakuu wa wilaya wakasaini na wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa, nao wakasaini wa maafisa watendaji wa kata. Maafisa watendaji wa kata wakasaini na maafisa watendaji wa mitaa. Hii inaonesha umuhimu wa masuala ya Lishe na afua zake katika jamii. Lengo kubwa ni kupunguza athari za utapiamlo katika jamii” alisema Nkelege.

Alisema kuwa huduma zilizotolewa katika maadhimisho hayo ni elimu ya Afya na Lishe, maonesho ya makundi matano ya vyakula na upikaji wake, upimaji wa Afya ukihusisha kupima HIV, uzito na urefu (BMI) pamoja na kutoa kutoa vyeti kwa watoto wadogo, matone ya Vitamin "A" na kupima MUAC kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano.

Afisa mtendaji huo alisema matarajio ya utekelezaji wa mkataba wa Lishe, alisema kuwa ni kuona hali ya lishe inabadilika na kuwa bora zaidi katika kata yake hasa kwa kina mama wajawazito, watoto wenye umri chini ya miaka mitano na vijana balehe.

Akiongelea maadhimisho hayo alisema kuwa ni utekelezaji wa kipengele namba mbili katika mkataba wa lishe linachoelekeza kata na mitaa kufanya maadhimisho ya siku ya afya na lishe ya mtaa (SALIKI) katika mitaa.

Maadhimisho ya siku ya Afya na Lishe ya Mtaa hufanyika kwa mitaa yote kila baada ya miezi mitatu na katika mtaa wa Mailimbili yaliongozwa na kaulimbiu isemayo “Lishe Bora kwa Ustawi wa Afya zetu na Maendeleo ya Mtaa wetu” ukiwa ni mtaa wa pili ukitanguliwa na mtaa wa Sokoine.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.