• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kata ya Chang'ombe yampongeza diwani wao, utatuzi kero za elimu na afya

Imewekwa tarehe: June 2nd, 2022

Na. Shaban Ally, DODOMA

KATA ya Chang'ombe imempongeza Diwani wake Mhe. Bakari Fundikira kwa juhudi zake za kuleta maendeleo katika kata hiyo kwa kutatua changamoto za afya na elimu.

Pongezi hizo zimetolewa na Mtendaji wa Kata ya Chang’ombe, Emmanuel Mazumila (aliyesimama pichani juu) wakati akimkaribisha diwani kufunga kikao cha Kamati ya Maendeleo ya Kata (WDC) kilichofanyika katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata leo tarehe 02 Juni, 2022.

Mazumila amesema kuwa anampongeza diwani wa kata hiyo kwa kutatua changamoto ya afya na elimu. Amesema kuwa diwani huyo amekuwa mstari wa mbele katika kufanikisha ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe na kuwaondolea kero ya kutembea umbali mrefu wananchi kufuata huduma za afya. Katika elimu alisema kuwa diwani huyo ameshiriki kuhimiza wazazi kuwapeleka watoto shule na kufuatilia maendeleo yao, aliongeza Mtendaji huyo.

Aidha, Mazumila amewashauri wananchi na wadau wa maendeleo katika Kata hiyo kuendelea kuheshimu na kuthamini juhudi zinazoendelea kufanywa na diwani wao katika kuwaletea maendeleo. Mtendaji huyo ameshauri jina la diwani huyo liwekwe kwenye moja ya barabara au mtaa katika kata yao kama wafanyiwavyo viongozi mbalimbali.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Chang’ombe, Mhe. Bakari Fundikira aliwashukuru viongozi na wananchi wa Kata ya Chang'ombe kwa pongezi walizompatia juu ya kazi kubwa anayoifanya ya kutatua changamoto zilizopo katika kata hiyo kwa muda mrefu. "Mimi binafsi nimepokea pongezi hizi kwa moyo mkunjufu kwa kuwa bila ya mshikamano wetu, sisi kama viongozi, hatuwezi kufanikisha masuala ya kimaendeleo," alisema Fundikira.

Kikao cha Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Chang’ombe kilihudhuriwa na Wenyeviti wa Mitaa, Mabalozi, wadau wa maendeleo na wajumbe. Pamoja na mambo mengine kikao kilijadili masuala ya afya na elimu katika kata hiyo.

Mheshimiwa Bakari Fundikira (katikati) akishukuru kwa pongezi alizopewa kutokana na juhudi zake za kutatua changamoto za upatikanaji wa huduma za afya na masuala ya elimu katika kata ya Chang'ombe.

Baadhi ya Wenyeviti wa Mitaa, Mabalozi, wadau wa maendeleo na wajumbe wa kikao cha Kamati ya Maendeleo ya Kata (WDC) kilichofanyika katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata leo tarehe 02 Juni, 2022.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.