• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kaya zenye Vyoo bora nchini zafikia 63.7%

Imewekwa tarehe: November 21st, 2020

MKURUGENZI wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi amesema kuwa, asilimia 63.7% ya kaya zote nchini Tanzania zimefanikiwa kuwa na vyoo bora kwa mwaka 2020, kutoka asilimia 59 mwaka 2019, huku lengo likiwa ifikapo mwaka 2030 kila mtu Duniani atumie choo bora.

Dkt. Subi amesema hayo juzi (Novemba 21, 2020) wakati akiongea na Waandishi wa habari katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma ikiwa ni siku ya matumizi ya choo Duniani na wiki ya usafi wa mazingira Tanzania.

"Kaya zenye vyoo bora zimeongezeka kutoka asilimia 59 mwaka 2019 hadi kufikia asilimia 63.7 mwezi Juni, 2020, huku lengo namba 6.2 la dunia la maendeleo endelevu limeweka bayana kila mtu Duniani anatakiwa kutumia choo bora huku likitanabaisha kuwa kufikia mwaka 2030 hakuna atakayejisaidia hovyo katika mazingira yasiyo rasmi". Amesema Dkt. Subi.

Amesema kuwa, Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “Zingatia Mahitaji ya Jinsia kwa Usafi wa Mazingira Endelevu” (Gender Consideration a Pillar for sustainable Sanitation and Hygiene), lengo likiwa ni kuongeza uelewa zaidi juu ya umuhimu wa kujenga na kutumia choo bora pamoja na kuweka mazingira safi wakati wote.

Aidha Dkt. Subi amesema kuwa, Mikoa inayoongoza kwa kuwa na asilimia kubwa ya kaya zenye vyoo bora ni pamoja na Dar es Salaam (95.8%), Iringa (77.5%) na Njombe (74.6%), huku akiweka wazi Mikoa yenye hali duni ni pamoja na Kigoma (49.3%), Lindi (49.2%) na Dodoma (46.1%).

"Mikoa inayoongoza kwa kuwa na asilimia kubwa ya kaya zenye vyoo bora ni Dar es Salaam (95.8%), Iringa (77.5%) na Njombe (74.6%). Mikoa yenye hali duni ni Kigoma (49.3%), Lindi (49.2%) na Dodoma (46.1%)" amesema Dkt. Subi.

Mbali na hayo, Dkt. Subi amehimiza Jamii ihakikishe inajenga na kutumia vyoo bora ili kuepuka kupata maambukizi ya magonjwa ya mlipuko na kuwataka kujenga tabia ya kunawa mikono pamoja na kuimarisha usafi wa mazingira ngazi ya kaya.

Hata hivyo, Dkt, Subi ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha wanatupa kinyesi cha watoto chooni pamoja na kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni.

Tovuti hii ilimtafuta Afisa Afya wa Jiji la Dodoma Abdallah Mahia ili kupata maelezo zaidi kuhusu hali ya vyoo katika Jiji la Dodoma ambapo alisema "Hali ya Vyoo bora katika Jiji la Dodoma hatuko kwenye nafasi mbaya, tuna asilimia 76.5 ya kaya zenye Vyoo bora. Kikubwa kilichofanya mkoa wa Dodoma kuwa na kiwango duni imechangiwa na baadhi ya Halmashauri ambazo kiwango chake cha kaya zenye Vyoo bora bado kiko chini sana hivyo kusababisha mkoa kushika nafasi ambayo si nzuri" alifafanua Mahia.

Aidha, Afisa Afya huyo wa Jiji aliwakumbusha wananchi wa mkoa wa Dodoma kujenga Vyoo kwa kutumia vifaa vya kudumu na kuezeka kwa kutumia kenchi (mbao na fito) badala ya kuweka bati au nyasi pekee na kupelekea mvua zinaponyesha Vyoo hivyo kuanguka na kubaki wazi sehemu ya juu na hivyo kupoteza ubora wa vyoo hivyo. Bwana Mahia amesisitiza kuwa jambo hili ni jukumu la kila mwananchi ili kuweka afya za Wanadodoma salama.


Dkt. Leonard Subi (wa pili kulia) wakati akiongea na Waandishi wa habari katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma ikiwa ni siku ya matumizi ya choo Duniani na wiki ya usafi wa mazingira Tanzania.

Afisa Afya wa Jiji la Dodoma Abdallah Mahia alipokuwa akitoa ufafanuzi kwa tovuti hii kuhusu hali ya Vyoo katika Jiji la Dodoma na sababu iliyosababisha Mkoa wa Dodoma kushika nafasi ambayo si nzuri kitaifa huku akiweka msisitizo kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma kujenga vyoo bora kwa afya zao.

Chanzo: Wizara ya Afya (Instagram), tovuti ya Jiji Dodoma

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.