• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kazi nzuri, ujenzi wa Kituo cha Afya Nkuhungu

Imewekwa tarehe: July 23rd, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KAMATI ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeridhishwa na ujenzi unaoendelea wa kituo kipya cha afya katika Kata ya Nkuhungu na kusema kuwa Kamati ya Ujenzi imetimiza wajibu wake.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango Miji na Mazingira, Jaffar Mwanyemba alipoongoza Kamati ya Fedha na Utawala ‘route one’ kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo kipya cha afya katika Kata ya Nkuhungu mwishoni mwa wiki.

Mwanyemba alisema kuwa wajumbe wameridhika na kazi nzuri iliyofanywa katika utekelezaji wa ujenzi wa majengo ya kituo hicho cha afya. Aidha, kamati zinazosimamia ujenzi huo zilipongezwa kwa kutimiza wajibu wake vizuri katika kusimamia taratibu za ujenzi wa kituo hicho cha afya.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa Kituo cha Afya Nkuhungu, Mwasiti Abdallah alisema kuwa ujenzi ulianza tarehe 17/3/2022 kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Lengo ni kutoa huduma bora na kwa wakati kwa wananchi baada ya kuwa na uhitaji wa huduma za afya katika kata na maeneo jirani. Jumla ya shilingi 207,996,246 zimepokelewa kwenye akaunti ya kata kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje na maabara. Hadi sasa majengo ya wagonjwa wa nje na maabara yamepauliwa. Miundombinu ya maji na umeme imeshasambazwa na shughuli za ukamilishaji wa majengo unaendelea na umefikia asilimia 70 ya utekelezaji” alisema Abdallah.

Alisema kuwa kiasi cha fedha kilichotumika ni shilingi 187,000,000. Baada ya awamu hii itafuata ujenzi wa majengo ya upasuaji, wodi ya wazazi na kichomea taka, aliongeza.

 Akiongelea faida za mradi, alisema kuwa ujenzi huo utakapokamilika utaisaidia jamii ya watu wapatao 38,622 kupata huduma za kliniki ya watoto karibu na jamii. Faida nyingine ni kuwezesha wananchi kupata huduma bora za afya katika kata ya nkuhungu kwa sababu kata hiyo haikuwa na kituo chochote cha serikali.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.