• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ugonjwa wa Kichaa cha Mbwa, unavyoenea, kinga na athari zake

Imewekwa tarehe: September 30th, 2019

Kichaa cha Mbwa ni ugonjwa wa kuambukiza unaoathiri mfumo wa kati wa fahamu yaani ubongo na Ugwe mgongo na kupelekea kupooza, kupoteza fahamu au kifo. Ugonjwa huu ni hatari na husabishwa na virusi viitwavyo kitaalam kitaalam kama rabies virus. Vijidudu hivi vinapatikana katika mate au damu ya binadamu na wanyama wengine kama mbwa, mbweha, paka, popo n.k.

Ufafanuzi huu umetolewa na Afisa Afya wa Jiji la Dodoma Abdallah Mahia leo alipokuwa akiongea na tovuti ya Jiji la Dodoma ili kutoa elimu na tahadhari kwa wakazi wa Jiji la Dodoma. Mahia amesema hatuna budi kuendelea kutoa elimu hii kwa wananchi wetu ili waweze kuchukua hatua mapema za kujikinga na madhara ya ugonjwa wa Kichaa cha Mbwa. "Ugonjwa huu hauna msimu, wakati wo wote unaweza kutokea, hivyo ni muhimu kila mwana Dodoma kuchukua tahadhari ya kujikinga" amesema Afisa Afya wa Jiji la Dodoma.

Ugonjwa huu husambaa na kuleta madhara zaidi kwa watoto ndani ya muda mfupi chini ya siku 10. Hii hutokana na kinga yao kutokomaa, vilevile watoto huwa karibu sana na wanyama wafugwao na hivyo kupelekea kuumwa au kugusa mate yao.

Tiba yake mpaka sasa haijapatikana kama ilivyo kwa magonjwa mengine ya virusi lakini kumekuwepo chanjo ambayo hutolewa kabla au baada ya kuambukizwa ili kuzuia kusambaa na kuleta madhara mwilini. Pamoja na chanjo kama dalili zikiwa zimeshajitokeza kupona huwa sio rahisi.

Kwa takribani miaka 30 iliyopita ni watu 7 tu walipona baada ya chanjo wakiwa na dalili. Kuna mikakati iliyopo ya Umoja wa Kimataifa kuutokomeza ugonjwa huu ifikapo mwaka 2030.

Kutokana na hali ya kiuchumi nchi zinazoathirika zaidi ni za Africa, hii ndio sababu kubwa ikiwemo Tanzania kushindwa kutokomeza kichaa cha mbwa ambapo inakadiriwa gharama ya chanjo yake kufikia sh. 150,000.

Unaenezwa vipi kwa Binadamu:

  • Kuumwa au kukwaruzwa na mnyama mwenye virusi hivi, ambavyo hupenyeza katika ngozi na kuingia mwilini. Madhara huonekana haraka zaidi kama majeraha yapo karibu na kichwa, 
  • Kugusana na mate ya wanyama na baadae kupitia mdomoni huweza kuingia mwilini, 
  • Kwa njia ya hewa kutoka kwa popo.
  • pia inaweza kuambukizwa kwa kugusa damu ya mnyama mwenye maambukizi ya virusi hivi. 

Tofauti na mbwa ambaye amezoeleka kuambukiza ugonjwa huu, pia wanyama kama paka, mbweha, mbwa mwitu na popo wanahusishwa kwenye kuambukiza ugonjwa huu.

Dalili za Kichaa cha mbwa kwa binadamu

Dalili za ugonjwa huanza kuonekana baada ya mwezi hadi miezi mitatu baada ya kung’atwa na mnyama mwenye maambukizi, lakini pia tafiti zinaonyesha kuwahi hadi wiki tatu baada ya kuambukizwa hadi miaka saba.

Dalili hizi ni kama:-

  • Homa na kuhisi uchovu mwa mwili.
  • Kichwa kuuma na kuchanganyikiwa
  • Kubadilika tabia kuwa mkali kupita kiasi
  • Kukasirika au kuogopa sana, hofu ya maji ‘hydrophobia’,
  • Kukosa uwezo wa kutawala mwendo wa viungo vya mwili
  • Kupoteza fahamu

Mara dalili hizi zinapoonekana maana yake ugonjwa umeshaanza kuharibu ubongo na neva na uwezekano wa mgonjwa kupona kunakuwa ni nadra sana na hivyo basi kifo huweza kutokea.

Matibabu na Kinga

Tiba ya chanjo kujikinga na maambukizi ya virusi hivi ikitolewa mapema au mara moja baada ya kuambukizwa, lakini tiba inahitaji kutekelezwa kabla virusi havijafikia ubongo, kwa hiyo ni muhimu kupata matibabu katika muda wa saa za kwanza baada ya kung’atwa.

Pia ni kutoa chanjo kwa mbwa wote ili kuwakinga na virusi hivi.

Ni muhimu wanyama wa kaya wapewe chanjo dhidi ya ugonjwa huu ili kulinda mbwa kutopata maambukizi ya virusi hivi.

Kuosha mahali palipo umwa au penye mchukubo kwa dakika 15 kwa maji na sabuni au povidoni/iodine, vinaweza kuua virusi pia na kuwa na ufanisi fulani katika kuzuia maambukizi ya kichaa cha mbwa.  



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.