• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kikundi cha Wenye ulemavu “Tujikubali” bado chahitaji msaada

Imewekwa tarehe: August 29th, 2021

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MWENYEKITI wa kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, Johnick Risasi ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuwawezesha watu wenye ulemavu kupata mikopo ya asilimia mbili kutoka mapato ya ndani.

Meja Mst. Risasi alitoa pongezi hizo alipoongoza Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Dodoma kutembelea kikundi cha watu wenye ulemavu cha TUJIKUBALI kilichopo Mtaa wa Nzuguni ‘B’ Kata ya Nzuguni, jijini Dodoma.

Meja Mst. Risasi alisema kuwa kitendo cha Halmashauri kuwakopesha watu wenye ulemavu ni kuonesha kuwajali watu hao. “Mheshimiwa Rais Samia anazungumzia usawa kwa watu wote. Watu wenye ulemavu wakiwezeshwa wanaweza kujiletea maendeleo. Ushauri, watu hawa watafutiwe sehemu nzuri na kuangalia jinsi ya kuwezeshwa kulipa pango. Huku wanapofanyia shughuli zao pamejificha sana” alisema Meja Mst. Risasi.

Mwenyekiti huyo alishauri viatu wanavyoshona viboreshwe zaidi kwenye umaliziaji ili kuwa na muonekano mzuri na wa kuvutia zaidi. “Nimefurahi sana kwa juhudi hizi. Uongozi wa Kata uwasaidie kufikia masoko na ikibidi wasaidiwe kupata Bajaji kwa ajili ya kurahisisha usafiri wao” alisisitiza Meja Mst. Risasi.

Akisoma taarifa fupi ya kikundi cha Tujikubali walemavu, Mweka Hazina, Pauleta Lesso (pichani juu) alisema kuwa miundombinu na usafiri ni changamoto. “Miundombinu na usafiri kwa sisi walemavu ni changamoto kubwa hasa wakati wa kutafuta masoko na kuuzia bidhaa zetu. Vile vile, uhaba wa masoko ya kuuzia viatu baada ya kutengeneza pia ni changamoto kwetu” alisema Lesso. Aidha, aliongeza kuwa kutawanyika kwa baadhi ya wanakikundi kutokana na sababu binafsi kumepelekea kupoteza uaminifu katika kikundi, aliongeza.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Rukia Bakari alisema kuwa halmashauri imepanga kujenga jengo kwa ajili ya shughuli za wajasiriamali eneo la Nzuguni. “Jengo hilo likikamilika litawawezesha wajasiriamali kuwa sehemu moja na inayofikika kirahisi kwa ajili ya kuuza bidhaa zao” alisema Bakari.

Nae Diwani kwa Kata ya Nzuguni, Aloyce Luhega alisema kuwa kikundi chicho kinakabiliwa na changamoto ya usafiri. “Tumeshawaombea usafiri kwenye mfuko wa Jimbo na bahati nzuri mheshimiwa Mbunge amelipokea vizuri. Mbunge ameahidi kuangalia katika bajeti yake kuona jinsi ya utekelezaji wake” alisema Luhega.

Mwenyekiti wa kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, Meja Mst. Johnick Risasi akiangalia moja ya bidhaa zinazotengenezwa na kikundi cha Tujikubali walemavu kilichopo kata ya Nzuguni Jijini Dodoma.

Baadhi ya bidhaa zinazotengenezwa na kikundi cha Tujikubali walemavu kilichopo Kata ya Nzuguni ambao ni miongoni mwa wanufaika wa mikopo ya asilimia 2 kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.