• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kiongozi wa Mbio za Mwenge aipongeza serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano

Imewekwa tarehe: October 3rd, 2023

Na. Dennis Gondwe, IPAGALA

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023, Abdalla Shaib Kaim ameipongeza serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo elimu nchini.

Pongezi hizo alizitoa alipoongoza Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 kutembelea, kukagua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi ya Dodoma English Medium katika Kata ya Ipagala jijini Dodoma.

Kaim alisema “niipongeze serikali ya awamu ya sita kwa kazi kubwa inayofanya ikiwa ni pamoja na kutenga na kutoa fedha nyingi za kutekeleza miradi ya maendeleo. Tumejiridhisha na nyaraka za mradi huu baada ya kuzikagua zipo vizuri sambamba na mradi nikiri mpaka hatua hii kazi kubwa na nzuri imefanyika. Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 tumeridhia uwekaji jiwe la msingi” alisema Kaim.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi ya Dodoma English medium kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prisca Myalla alisema kuwa lengo la kujenga shule hiyo ni kutoa elimu bora zaidi ambayo itasaidia kupata wataalam mbalimbali kwa maendeleo ya kiuchumi. “Lengo lingine ni kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia, kuongeza uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali na msingi na kuwezesha wananchi wa kipato cha kati kupata fursa ya kuwapeleka watoto katika shule ya mchepuo wa kiingereza inayomilikiwa na Serikali” alisema Myalla.

Alisema kuwa halmashauri ilipokea shilingi 400,000,000 tarehe 20 Aprili, 2023 kutoka serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa shule ya awali na msingi. Halmashauri ya Jiji Dodoma imetoa shilingi 58,316,799 kupitia mapato ya ndani kusaidia ujenzi huo. “Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023, utekelezaji wa mradi huu ulianza rasmi tarehe 05.05.2023.     Tumefanikiwa kujenga Jengo la Utawala, vyumba 11 vya madarasa, ikiwa madarasa 02 ni kwa ajili ya Elimu ya Awali na madarasa 9 kwa ajili ya darasa la I hadi la VII. Aidha, yamejengwa matundu 38 ya vyoo, matundu 6 ni kwa ajili ya wanafunzi wa elimu ya Awali na 32 kwa ajili ya elimu ya msingi. Hadi sasa mradi upo hatua za umaliziaji. Miti 200 imepandwa kati ya hiyo, Miti 100 ni ya matunda na Miti 100 ni kwa ajili ya kivuli” alisema Myalla.

Akiongelea gharama za mradi huo, alisema kuwa umetumia shilingi 330,882,100 na unatarajia kukamilika tarehe 31 Oktoba, 2023.

Kuhusu mafanikio ya mradi, alisema kuwa utatoa huduma ya elimu ya mchepuo wa kiingereza na kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule zenye upungufu wa vyumba vya madarasa. “Mafanikio mengine ni kuleta huduma ya elimu karibu na jamii, kuongeza ufaulu kwa wanafunzi katika suala zima la kitaaluma kutoka asilimia 89.9 kwa mwaka 2022 na kufikia asilimia 100 na kuhamasisha jamii juu ya utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti” alisema Myalla.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.