• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa ampongeza Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: August 17th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2022 Sahili Geraruma amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kutekeleza agizo la Rais kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Pongezi hizo alizitoa baada ya kutembelea mradi wa kilimo wa kikundi cha Kiu ya Ufanisi na kuridhishwa na utekelezaji wa mradi huo unaotekelezwa kwa mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Geraruma alisema kuwa Halmashauri ya Jiji inakopesha fedha vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Alishauri kuwa fedha hizo zinazokopeshwa kwa vikundi zitumike kufanya shughuli za maendeleo.

“Nimpongeze Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa halmashauri kutoa mikopo isiyo na riba kwa makundi hayo. Nitoe rai kwamba watanzania wote wenye sifa watakaokuja kukopa wapewe mikopo” alisema Gararuma.

Aidha, aliwataka wakopaji wa mikopo hiyo kuirejesha kwa wakati ili wakopaji wengine waweze kupata fursa ya kukopa. “Mimi nimependezwa na kazi inayofanywa na vijana wenzangu, endeleeni kwa mujibu wa malengo mliyojiwekea” alisema Geraruma.

Akisoma taarifa ya mradi wa kilimo wa kikundi cha Kiu ya Ufanisi kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2022, Mwenyekiti wa kikundi, Onesmo Mnyamagola alisema kuwa kikundi hicho kilikopa ili kuwezesha wanakikundi kujiajiri na kuweza kuendesha maisha yao na kununua vitendea kazi.  

Alisema kuwa mradi huo ulinunua kitalu nyumba kwa shilingi 14,234,000.00. Vitu vingine vilivyonunuliwa ni “pampu shilingi 5,500,000.00 kusafisha kisima kwa shilingi 1,200,000.00, ununuzi bomba za maji za plastiki (PVC pipe)  rola moja shilingi 850,000.00, ununuzi wa nyaya za kupeleka umeme kwenye pampu mita 200 shilingi 2,400,000.00 ununuzi wa mfumo wa umwagiliaji shilingi 3,527,000.00, ununuzi wa pembejeo kama mbolea, mbegu, kamba za kufungia nyanya na viuatilifu shilingi 2,020,000.00, ununuzi wa miti shilingi 3,250,000.00, ununuzi wa samadi shilingi 600,000.00, chombo cha usafiri shilingi 3,050,000.00 na ununuzi wa vitendea kazi shilingi 1,200,000.00” alisema Mnyamagola.

Alisema kuwa baada ya kupata mkopo wamefanikia mambo kadhaa. “Kupitia mkopo huu tumefanikiwa kukamilisha lengo kuu la kutengeneza kitalu nyumba, kufunga mifumo ya umwagiliaji pamoja na kuajiri vijana watatu katika shughuli za mradi na kuongeza mapato ndani ya Serikali kwa kulipa kodi kupitia manunuzi mbalimbali” Mnyamagola.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.