• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kirusi cha India balaa, hatua zichukuliwe kuikabili Korona - Wataalam

Imewekwa tarehe: May 7th, 2021

WATAALAM wamesema aina mpya ya virusi vya korona ‘double mutant’, ambavyo vimeonekana nchini India ni hatari zaidi kutokana na uwezo wake wa kubadilika mara kwa mara.

Kirusi hicho kipya aina ya B.1.617 ndicho kinaelezwa kuwa wimbi la pili kuipiga India, ambayo imeshuhudia maambukizi kufikia zaidi ya milioni 21 huku vifo vikifikia 230,168 hadi kufikia jana mchana.

Mtaalam wa maikobaolojia na virusi kutoka Chuo Kikuu cha Muhimbili (MUHAS), Dkt. Joe Manyai amesema aina hiyo ya kirusi kina tabia ya kujibadilisha mara kwa mara.

“Kirusi hicho hicho kinajibadilisha kidogo kinachukua chembechembe nyingine ya jeni (gene) inatengeneza rangi nyeupe kidogo au hufifia na hujiweka kwa binadamu au mnyama.

Kina tabia ya kutumia protini, kinajibadilisha kidogo ili kuwa orijino, kinajibadilisha mara mbili, kama kilikuwa A kinabadilika kuwa B halafu baadaye kinakuwa C, kikifanya mabadiliko kinakuwa kirusi kingine ili kiweze kuenea kwa urahisi zaidi,” alisema Dkt. Manyahi.

Wakati wanasayansi wakiwa katika uchunguzi kuhusu aina mpya ya kirusi cha Korona kinachoua nchini India, wataalam wa afya nchini wametoa angalizo huku wakijata mbinu mbalimbali zitakazosaidia kuepukana na kirusi hicho.

Madaktari wameiomba Serikali kupunguza mwingiliano wa watu, kuongeza upimaji na pia taasisi zenye uwezo ziruhusiwe kupima na nchi iandae hospitali za dharura zenye oksijeni za kutoka. Wameonya kuwa Tanzania inapaswa kuwa makini na kupata fundisho kutokana na wimbi la Korona nchini India.

Daktari bingwa wa magonjwa ya ndani na yanayoambukiza kutoka Hospitali ya Aga Khan, Mandela Makalala alisema virusi vya Korona vinabadilika badilika sana na vinaweza kuwa hatari zaidi ya tunavyofikiria kwa kuongezeka uwezo wa kusambaa zaidi na makali ya ugonjwa.

Alisema yatupasa kujitathmini kama nchi tumejiandaa vipi kupambana na wimbi la Korona litakalokuja.

“Madaktari tulio wengi tunadhani ni muhimu kuanza kutoa chanjo kwa makundi yaliyo katika hatari kubwa, yaani watumishi wa afya, wazee na wagonjwa wenye matatizo ya kiafya kama sukari, shinikizo la damu, magonjwa ya moyo na uzito kupita kiasi” alisema Dkt. Makalala.

Dkt. Makalala alisema ni muhimu kupunguza mwingiliano wa watu katika nchi ambazo zina wagonjwa wengi wa Korona na sisi Tanzania kama nchi tunahitaji kuongeza upimaji wa virusi vya Korona, kwa sasa ni maabala ya Taifa inayopita virusi hivyo. 

“Turuhusu taasisi binafsi zenye uwezo wa kupima, hii itaongeza kasi ya kutambua maambukizi mapema na hivyo kuyapunguza. Inasikitisha na kuumiza moyo unapomwambia mgonjwa hospitali imejaa. Hili lilitokea katika awamu (wave) zote mbili za Korona hapa Tanzania, tusingelipenda kuliona tena” alisema Daktari huyo.

Chanzo: Gazeti la Mwananchi

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.