• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kiswahili lugha rasmi ya SADC

Imewekwa tarehe: August 18th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametangaza uamuzi wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC kuwa lugha ya Kiswahili inakuwa lugha rasmi ya 4 ya SADC kuanzia leo tarehe 18 Agosti, 2019.

Mhe. Magufuli ametangaza uamuzi huo wakati akifunga Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika kwa siku 2 (tarehe 17-18 Agosti, 2019) katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar Es Salaam.

TANZANIA imekabidhiwa rasmi uenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) huku ikijivunia lugha yake ya Taifa, Kiswahili kupitishwa rasmi kuwa moja ya lugha itakayotumika katika shughuli rasmi za jumuiya hiyo.

Awali, Kiswahili kilitangazwa rasmi kuwa lugha ya nne ya jumuiya hiyo Dar es Salaam jana na aliyekuwa Mwenyekiti wa SADC ambaye pia ni Rais wa Namibia, Dk Hage Geingob alipohutubia Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa jumuiya hiyo kabla ya kukabidhi madaraka kwa Mwenyekiti mpya, Rais wa Tanzania, Dk John Magufuli.

Ni faraja kwa Watanzania wote kwa kuwa, ndiyo lugha ya Taifa lao. Ni kutakana na sababu hiyo, muda mfupi kabla ya kukabidhi madaraka kwa Rais Magufuli kuelekea hitimisho la hotuba yake, iliufanya ukumbi kulipuka kwa vigelele na shangwe hasa kutoka kwa wananchi wa Tanzania waliokuwa wengi kutokana na kuwa wenyeji wa mkutano.

Nchi 16 zinazounda SADC zimekuwa zikitumia lugha tatu ambazo ni Kiingereza, Kireno na Kifaransa, hivyo kurasmisha lugha ya Kiswahili, kunaifanya jumuiya hiyo kuwa na lugha nne.

Watanzania, mbali na kujivunia kushika kijiti cha uenyekiti kwa kipindi cha mwaka mzima, lakini pia inatia faraja kubwa kuona lugha ya Kiswahili imepata nafasi hiyo kubwa na ni kati ya vipaumbele ambavyo Serikali imeviainisha wakati ikichukua kijiti hicho.

Ndiyo maana baada ya kutangazwa, hali katika Ukumbi wa Selous wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), ikabadilika huku baadhi ya washiriki wa ufunguzi huo wakishangilia kwa kusimama na kuungwa mkono na watu wengi (wasio Watanzania) waliohudhuria tukio hilo.

Pia kwa msisitizo wa furaha hiyo, Rais Magufuli akajikuta mbali na kuanza kuzungumza kwa lugha ya Kingereza iliyozoeleka, akimalizia hotuba yake kwa lugha ya Kiswahili, kwanza kama Rais wa nchi inayozungumza lugha hiyo, hivyo kufunga pazia rasmi, lakini pili kama mwenyekiti mpya ambaye angependa kuona lugha hiyo inaanza kwa kasi ikianzia pake alipokabidhiwa kijiti jana.

Kama alivyosema Rais Magufuli, lugha ya Kishwahili ina historia yake katika jumuiya ya baadhi ya nchi za SADC, moja ikiwa ni jinsi ilivyotumika kama lugha ya ukombozi wakati wa harakati za kutafuta uhuru kwa nchi nyingi za Afrika.

Dk Magufuli akasema wakati akikabidhiwa kijiti hicho kuwa mapambano ya ukombozi wa Afrika yalifanikiwa na nchi zote za Afrika katika miaka ya 1990 zilipata uhuru moja ya sababu ikiwa ni matumizi ya Kiswahili.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli, Kiswahili ni lugha ya 10 duniani kuzungumzwa na watu wengi na ya 13 Afrika na ya sita katika nchi za SADC.

Akasema ni lugha rasmi Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na ni lugha rasmi kwa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).

Ikumbukwe kwamba Rais Magufuli pia alipofungua Maonesho ya Nne ya Wiki ya Viwanda, alitoa hutuba yake kwa Kiswahili kudhihirisha umuhimu wa lugha hiyo iliyotumiwa na wapigania uhuru wa nchi za kusini mwa Afrika kwa ukombozi. Kufikia hapo, ni kazi kubwa imefanyika.

Pongezi ziwaendee pia wanaounda Baraza la Mawaziri la SADC ambao, katika mapendekezo yao 107 waliyoyawasilisha kwenye mkutano huo wa 39 wa wakuu wa nchi na serikali wa jumuiya hiyo kwa uamuzi, Kiswahili kilikuwa ni mojawapo.

Bofya hapa kusoma taarifa rasmi ya Ikulu: Taarifa ya SADC.pdf


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya na Maendeleo Kusini mwa Africa (SADC) akiongoza kikao cha ndani cha Wakuu wa Nchi na Serikali za Jumuiya hiyo. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Jumuiya Dkt. Taxs.

Chanzo: Mitandao na tovuti ya habarileo.go.tz

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.