• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kituo cha Afya Changombe kuhudumia watu 30,024 Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: August 17th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MRADI wa ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe unatarajia kuhudumia wakazi 30,024 kwa kuwapatia huduma bora za afya na kuboresha maisha yao.

Kauli hiyo ilitolewa na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2022 katika kituo hicho cha afya kilichopo Kata ya Chang’ombe jijini hapa.

Dkt. Method alisema “mradi huu utakapokamilika utasaidia wakazi wa Kata ya Chang’ombe kupata huduma za afya kwa ukaribu na kuboresha afya za wakazi wa kata hii. Jumla ya wakazi 30,024 watapata huduma bora za afya ambapo awali eneo hili lilikuwa halina kituo cha serikali kwa ajili ya kutoa huduma afya”.

Alisema kuwa mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe ulianza tarehe 24/12/2021 kwa fedha za tozo kutoka Serikali Kuu. “Mradi huu umepokea fedha kwa awamu mbili. Awamu ya kwanza ulipokea shilingi 250,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD), Maabara na kichomea taka. Awamu ya pili mradi ulipokea shilingi 250,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa jengo pacha la mama na mtoto na upasuaji, kujenga jengo la kufulia na kujenga njia za kuunganisha majengo hayo (walkways). Pia Halmashauri ya Jiji imetoa shilingi 103,272,633.00 kwa ajili ya samani na vifaa tiba kupitia mapato ya ndani” alisema Dkt. Method.

Akihusianisha mradi huo na ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2022, alisema mradi una uhusiano wa moja kwa moja. “Mradi huu unauhusiano na ujumbe wa Mwenge wa Mwaka 2022 unaosema Sensa ni Msingi wa Mipango ya Maendeleo; Shiriki kuhesabiwa tuyafikie maendeleo ya Taifa. Hivyo, basi zoezi la Sensa litasaidia kujua idadi ya sasa ya wakazi wa maeneo yatakayohudumiwa na kituo hiki ili kuwezesha kupanga mahitaji sahihi ya wananchi ikiwemo mahitaji ya dawa na vifaa tiba. Kwa sasa mradi huu utakapokamilika utatoa huduma kwa wakazi wapatao 30,024 wa Kata ya Chang’ombe na maeneo ya jirani” alisema Dkt. Method.

Kuhusu malengo ya mradi, alisema kuwa mradi umelenga kuboresha na kusogeza huduma za afya kwa jamii. Mradi unalenga kuwapunguzia akina mama wajawazito umbali mrefu wa kupata huduma za kujifungua. “Malengo mengine kusogeza huduma za kliniki ya watoto chini ya miaka mitano na kupunguza vifo vya akina mama na watoto wakati wa kujifungua, pamoja na kutoa huduma za upasuaji, aliongeza.

Kwa upande wa mwananchi, Zuhura Nia alisema kuwa kituo hicho kitakapokamilika ni msaada mkubwa kwao. Wanufaika wakubwa wa kituo hicho ni kina mama na Watoto ambao wamekuwa wakitembea umbali mrefu kutafuta huduma hizo.

Ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe unafanywa na mafundi wa ndani (Local fundi) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Chang’ombe na kusimamiwa na Wataalam kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.