• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kituo cha afya Chang’ombe kuboresha huduma za afya Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: May 11th, 2022

Na. Mwandishi Wetu, DODOMA

Kituo cha Afya Chang’ombe kuhudumia wakazi 25,415 wa Kata hiyo kitakapokamilika na kuwaondolea wananchi usumbufu wa kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya kituo cha Afya Makole jijini Dodoma.

Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikira alipokuwa akiongelea hatua za mwisho za ujenzi wa kituo hicho cha afya cha aina yake kinachojengwa katika Mtaa wa Msamaria, Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Diwani Fundikira alisema “mpaka sasa hatua ya ujenzi imefikia asilimia 98 na ujenzi umeenda vizuri kwa kuwa wataalam wa ujenzi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamekua wakikagua maendeleo ya ujenzi katika kituo hicho. Nimshukuru Mkurugenzi wa Jiji, Joseph Mafuru amekuwa mstari wa mbele katika kutafuta wataalam kwa ajili ya kukagua kituo hiki ili kiwe katika hali bora na usimamizi mzuri”.

Alisema kuwa kutokana na ukubwa wa kituo hicho, kinatarajia kuhudumia kata nne za jirani. “Kituo cha Afya Chang’ombe kinaweza kuhudumia wananchi wapatao 25,415 hii ni kwa mujibu wa  Sensa ya watu na makazi iliyofanyika Mwaka 2012, lakini pia kituo hiki kinatarajia kupokea wananchi wengine kutoka maeneo ya jirani kama vile Kata ya Mnadani, Miyuji, Chamwino, Nkuhungu na Kata nyinginezo ambazo hazina kituo kikubwa cha Afya. Hivyo, basi kituo hicho kitapunguza msongamano wa watu kwenye vituo vingine vya Afya na  hata Hospitali ya Mkoa almaarufu General” alisema Diwani Fundikira.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Chang’ombe, Dalia Kapinga aliwataka wakazi wa kata hiyo kukilinda na kukitunza kituo hicho ili kiweze kuwahudumia watu wengi zaidi. “Gharama zilizotumika katika ujenzi wa kituo hiki ni kubwa, hivyo natoa wito kwa wananchi kukilinda na kukitunza ili kiweze kudumu na kuhudumia watu wengi na kwa muda mrefu” alisema Kapinga.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Msamaria, Mwanaisha Matimbwa alisema kuwa wananchi wake walikuwa wakilazimika kufuata huduma za afya katika Kituo cha Afya Makole kilichopo mbali. “Hivyo, kupelekea shida pindi inapotokea kuna mgonjwa anahitaji huduma ya haraka na ukizingatia kituo cha Afya hakuna katika eneo la Chang'ombe” alisema Matibwa.

Ikumbukwe kuwa serikali kuu ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 250 fedha za tozo kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho katika Mtaa wa Msamaria zilizojenga jengo la wagonjwa wa nje na maabara na kufikisha idadi ya vituo vya afya vya serikali kuwa vitano katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.