• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kituo cha Afya Makole chapongezwa kwa kutoa huduma bora za tiba kwa wananchi

Imewekwa tarehe: June 5th, 2019

Serikali imekipongeza Kituo cha Afya cha Makole kilichopo katika jiji la Dodoma kwa jitihada zake za kuboresha huduma za tiba, na kupelekea ongezeko kubwa la wateja kutoka 25,480 waliokuwa wakipata huduma kituoni hapo miezi mitatu iliyopita  hadi 35,486 kufikia mwezi aprili mwaka huu sawa na ongezeko la wateja wapya 10,926 ambao ni sawa na ongezeko la asilimia 30.

Sambamba na ongezeko hilo, katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita idadi ya wateja waliokuja kupata matibabu katika kituo hicho wanaotumia Bima ya Afya (NHIF) imeongezeka kutoka wateja 470 hadi 973 ambao ni karibu maradufu ya wateja waliokuwa wakipata matibabu katika kituo hicho.

Akizungumza na wafanyakazi wa kituo cha Afya Makole, wakati wa ziara yake ya pili kukitembelea kituo hicho, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt Dorothy Gwajima ameelezea furaha yake kufuatia kupokea taarifa ya kituo hicho na Mganga Mfawidhi Dkt George Matiko, ambayo imeonyesha kuwepo kwa mabadiliko makubwa ya utoaji huduma kituoni hapo.

Dkt Gwajima amesema kuwa ikiwa ni miezi mitatu tangu alipofanya ziara yake kwa mara ya kwanza katika kituo hicho, mnamo Februari 17, mwaka huu, safari hii amefurahi kuona namna watendaji wa kituo hicho wakiongozwa na mlezi wa kituo hicho Bi Mary Shadrack walivyojidhatiti kutoa huduma bora za tiba kwa wananchi.

Amesema kitendo cha watumishi wa Kituo cha afya Makole kubadilika na kutoa huduma bora kwa wananchi kinapaswa kuigwa na vituo vyote vya kutolea huduma za afya nchini.

“Nilipotembelea kituo hiki tarehe 17 Februari, 2019, nilikuta kituo chenu kikiwa na malalamiko mengi ya wagonjwa hasa kero ya foleni na malalamiko ya kutoa huduma mbovu kwa wagonjwa, lakini sasa mmebadilika hongereni sana,” amesema Dkt Gwajima na kuongeza:

“Napenda kuwasihi muendelee na ari hiyo ya kutoa huduma kwani wananchi wengi wangependa kupata huduma katika vituo vya afya vya umma lakini wanakatishwa tama na huduma na mazingira mabovu wanayoyakuta.”

Kufuatia mafanikio hayo ambayo yamepatikana katika kipindi kifupi, Dkt Gwajima ametaka vituo vyote vya kutolea huduma za afya nchini viige mfano wa kituo cha afya Makole.

Wakati huo huo Dkt Gwajima amewapongeza Makatibu Tawala wa mikoa ya Morogoro na Ruvuma kwa kufanyia kazi taarifa za ziara zake katika mikoa hiyo na matokeo yake viongozi hao kuamua kufanya  mabadiliko kwa timu za usimamizi huduma za afya za mikoa yao jambo ambalo litaleta mabadiliko yatakayosaidia kuongeza kasi ya usimamizi kwa watendaji wapya watakaoteuliwa badala ya ule wa mazoea kama ulivyojidhihirisha kwa wajumbe walioondolewa.

Amesema katika mkoa wa Morogoro, katibu Tawala wa mkoa huo amelazimika kuwapumzisha wajumbe 9 wa Timu ya Uendeshaji Huduma za Afya Mkoa huo majukumu yao ya uongozi wa afya ili wakaendelee na majukumu ya kitaaluma katika vituo walivyopangiwa.

Wajumbe walioondolewa ni Dkt. Frank Jacob (Mganga Mkuu wa Mkoa) (RMO), Santiel Kinyongo (Mratibu wa Afya ya Uzazi na Mtoto) (RRCHCO), Salanga Maftah (Mratibu wa Huduma za Maabara) (RLT), na Florence Saka (Mratibu wa Malaria) (RMIFP).

Wengine ni Dkt. Emanuel Tenga (Mratibu wa Kifua Kikuu na Ukimwi) (RTB/HIV), Leticia Nchia (Mratibu wa Huduma za Ukimwi) (RACC), Dkt. Samson Tarimo (Mratibu wa Afya ya Kinywa na Meno) (RDO), Grace Masawe (Muuguzi Mkuu wa Mkoa) na Dkt. Secondry Njau (Mratibu wa Afya ya Macho) (REC).

Aidha, Wajumbe wengine 6 wa Timu ya Afya Mkoa wa Morogoro wamepewa onyo la kuboresha utendaji wao vinginevyo nao watatolewa kwenye nafasi za uongozi mara moja. “Ukipewa nafasi ya uongozi wa afya ngazi ya mkoa na halmashauri usimamie, ufuatilie na uchukue hatua au utoke kwenye nafsi hiyo na siyo vinginevyo,” amesema Dkt Gwajima.

Pia Dkt Gwajima amesema Timu ya Usimamizi Huduma za Afya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, Mkoani Singida na Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma pia, wajumbe wake wote wa kudumu wameondolewa kwenye nafasi zao za uongozi kutokana na uwajibikaji wa mazoea.

Katika ziara hiyo, Dkt Gwajima aliongozana na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt James Kiologwe na Mjumbe wa timu ya usimamizi na uendeshaji wa huduma za afya mkoa wa Dodoma Bi Mary Shadrack ambaye alipewa jukumu la kulea kituo hicho kwenye kipindi hiki cha maboresho.

Chanzo: tovuti ya OR-TAMISEMI (www.tamisemi.go.tz)

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.