• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kituo cha pili kwa ukubwa cha Polisi kujengwa Kata ya Chang'ombe

Imewekwa tarehe: June 23rd, 2021

KATIKA kukabiliana na matukio ya uhalifu ikiwemo uporaji, ukabaji na udhalilishaji, Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limedhamiria kujenga Kituo cha Polisi katika Kata ya Chang’ombe ambapo mpaka kukamilika kwake kinatarajiwa kugharimu Shilingi Milioni 130.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mshauri Mkuu wa Miradi ya Ujenzi ya Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi, Richard Malika wakati wa kupokea jumla ya matofali 6700 yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka ikiwa ni jitihada za mkuu wa mkoa huyo kukabiliana na matukio ya uhalifu yaliyoshamiri katika Kata ya Chang’ombe huku Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ikitoa kiasi cha Shilingi Milioni 10 katika kuchangia ujenzi huo.

“Tunakadiria hadi kukamilika kwa kituo hiki  jumla ya Shilingi Milioni 130 zitakua zimetumika kama gharama yam ujenzi wa jengo ukiachana na samani za ofisi na kitakua kituo cha pili kwa ukubwa kwa hapa Dodoma sambamba na kuzingatia haki za binadamu huku kila mahabusu zikiwa na sehemu ya choo na mabomba ya maji” alisema Naibu Kamishna Malika

Naibu Kamishna Malika pia aliwataka wahalifu pindi kituo hicho kitakapokamilika watafute taratibu nyingine za maisha kwani uhalifu sio kazi nzuri huku akiweka wazi kituo hicho kitakamilka ndani ya miezi sita.

Akizungumza baada ya makabidhiano ya matofali hayo, Diwani wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikira alisema wanaishukuru Wizara, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde ambae amechangia mifuko mia moja ya saruji katika mradi huo.

“Uhalifu hapa kwetu umekua ni changamoto watu wanaporwa wanafanyiwa matendo ya kihalifu lakini viongozi tumeanza mipango kukomesha uhalifu huo ikiwemo dhana ya ulinzi shirikishi na sasa ujenzi wa kituo hiki utaenda kukomesha matendo ya uhalifu katika maeneo ya Chang’ombe, sisi kama viongozi tutahakikisha tunawahamasisha wananchi wetu wachangie katika mradi huu na tunawashukuru wahisani wote waliotuunga mkono na wanaoendelea kutuunga mkono katika ujenzi huu”alisema Diwani Bakari.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.