• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

K’Ndege inatekeleza ujenzi wa zahanati

Imewekwa tarehe: July 14th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KATA ya Kiwanja cha Ndege inatekeleza ujenzi wa zahanati uliofikia hatua ya lenta ili kuwasogezea wananchi wake huduma za matibabu karibu na kuwaondolea usumbufu wa kufuata huduma hizo mbali.

Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Afisa Mtendaji wa Kata ya Kiwanja cha Ndege, Ashura Iberi mbele ya Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilipofanya ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa ujenzi wa zahanati hiyo mwishoni mwa wiki.

Iberi alisema kuwa kata yake ilipokea shilingi 40,000,000 kwa awamu tatu kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa awamu ya kwanza walipokea shilingi 10,000,000 zilizotumika kuseti jengo, kuchimba msingi, kumwaga zege la awali la msingi na kujenga tofali za msingi. “Awamu ya pili ilipokea shilingi 10,000,000 zilizofanya kazi ya kujaza kifusi, kupanga mawe, kusuka nondo na kumwaga zege la jamvi. Kazi nyingine ni kujenga ukuta wa kozi 10 na kufunga mbao za pembezoni mwa jamvi na utandazaji wa DPM, kufukia, kuondoa mbao na kumwagilia maji” alisema Iberi.

Kaimu Afisa Mtendaji huyo alisema kuwa awamu ya tatu walipokea shilingi 20,000,000 zilizotumika kununua vifaa vya ujenzi na kumlipa fundi. “Kazi zilizobaki ni kupaua, kutengeneza mfumo wa maji safi na taka, kuchimba bomba za umeme, kufitisha madirisha, kupiga plasta, blundering na kufunga bodi, skiming, kutengeneza sakafu ya kupokea vigae, rangi na kufunga milango na vitasa” alisema Iberi.

Mtendaji huyo alimshukuru Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma na Kamati yake ya Fedha na Utawala kutembelea na kukagua ujenzi huo. “Tunatoa shukrani pia kwa Mkurugenzi wa Jiji kwa kutupatia fedha kwa ajili ya ujenzi wa zahanati na Mhandisi Nicodemus Kileo kwa kutupatia ushirikiano wa karibu katika kazi zote zinazoendelea. Pia Diwani na Kamati ya Maendeleo ya Kata, Kamati ya Manunuzi, Mapokezi na Ujenzi na watendaji wote wa mitaa na wataalam kwa ushauri na usimamizi mzuri” alisema Iberi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe aliagiza iandaliwe ‘BOQ’ itakayoonesha gharama ya mradi wote hadi utakapokamilika. Alisema kuwa ‘BOQ’ itaiwezesha halmashauri kujua kiasi cha fedha kinachohitajika ili kinapotolewa kiwe na tija zaidi.

Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilifanya ziara ya kikazi kiutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi iliyotekelezwa na jiji hilo kwa kipindi cha robo ya nne (Aprili-Juni, 2022).

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.