• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kongole DOYODO mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia, yatimiza miaka 5

Imewekwa tarehe: December 6th, 2020

TAASISI ya Maendeleo ya Vijana Dodoma imepongezwa kwa kupambana kikamilifu na masuala ya ukatili wa kijinsia kwa wasichana katika kupunguza na kutokomeza mimba za utotoni.

Hayo yamesemwa jana na Mgeni rasmi wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Mhe. Dkt. Binilith Mahenge ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mhe. Josephat Maganga. Maadhimisho hayo yaliambatana na kauli mbiu isemayo “Tupinge ukatili wa kijinsia; mabadiliko yanaanza na mimi”.

“Naipongeza sana Taasisi ya DOYODO kwa kupambana kikamilifu na masuala ya ukatili wa kijinsia kwa wasichana hasa katika kupunguza na kutokomeza mimba za utotoni hapa jijini Dodoma” alisema Mhe. Maganga.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa DOYODO ndugu Rajabu Juma Suleiman aliongea wakati wa maadhimisho hayo aliishukuru Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kutambua jitihada zinazofanywa na SHirika la DOYODO na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali na wadau mbalimbali kwenye masuala ya maendeleo ya vijana jijiini Dodoma na kwa taifa zima kwa ujumla.

Aidha, Mkurugenzi Rajabu aliwapongeza vijana wa DOYODO kwa kutimiza miaka mitano ya kishindo tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo maarufu sana Jijini Dodoma.

Akifafanua zaidi kuhusu DOYODO Rajabu alisema kuwa, taasisi hiyo ilianzishwa rasmi mwaka 2014 ikiwa kama Umoja wa Vijana Dodoma (UWAVIDO) ambapo ilianza na vijana wasiopungua 40. Mwaka 2015 ilisajiriwa kisheria kama taasisi isiyo ya kiserikali (NGO) na kuwa Taasisi ya Maendeleo ya Vijana mkoani Dodoma (DOYODO).

Tangu kuanzishwa kwake DOYODO imekuwa na lengo la kuwajengea vijana uwezo kwenye maeneo ya elimu, uchumi, afya na uongozi, vilevile  imekuwa ikifanya jitihada kuhakikisha vijana wananufaika na fursa mbalimbali za maendeleo katika Mkoa wa Dodoma. Vijana walengwa ni wenye umri wa kuanzia miaka 10 hadi 24 ikijumuisha vijana waliopo mashuleni na hata nje ya shule. Katika kipindi cha miaka mitano tangu kuanzishwa kwake DOYODO imefanikiwa kuanzisha na kutekeleza mradi wa kuwajengea uwezo mabinti ili waweze kutimiza ndoto zao, mradi huo unaitwa “Magauni Manne Girls Empowerment Project”.

Mkurugenzi Mtendaji Rajabu alisema hivi sasa taasisi hiyo ina vijana takribani 130 ambao wanatoka katika vikundi vya vijana kwenye kata na mashuleni na taasisi ina viongozi saba hivi sasa.

Picha na matukio mbalimbali:

Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Josephat Maganga aliyemwakilisha Mgeni Rasmi Dkt. Binilith Mahenge akikabidhiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa DOYODO cheti cha heshima kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Dkt. Binilith Mahenge  ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake wa kuwasaidia vijana kunufaika na fursa zilizopo mkoani Dodoma.




Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mhe. Josephat Maganga (wa pili kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa DOYODO Rajabu Suleiman aliyesimama wakati akielezea kuhusu DOYODO na maendeleo ya Mradi wa Magauni Manne.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.