• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kongole Jiji la Dodoma kwa miradi ya kimkakati - DED Mkuranga

Imewekwa tarehe: December 24th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepongezwa kwa jinsi inavyotekeleza miradi ya kimkakati katika jitihada zake za kusogeza huduma karibu na wananchi na kukuza uchumi wa Jiji hilo.

Pongezi hizo zilitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Mhandisi Mshamu Munde baada ya kukamilika kwa ziara kutembelea miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma jana katika soko kuu la Ndugai linalojengwa jijini hapa.

Mhandisi Munde alisema kuwa lengo la ziara hiyo na timu yake ya wataalam ni kujifunza na kubadilishana uzoefu katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati. “Tumejifunza sana, nashukuru wataalam wa Halmashauri ya Jiji hili mmetutembeza na kutueleza kwa kina namna mnavyotekeleza miradi hii. Siwezi kusita kutoa pongezi kwa namna miradi hii inavyotekelezwa na pia inavyosimamiwa. Ushirikiano tumeona ni mkubwa. Hata wasilisho tulilopewa ofisini lilikuwa fasaha” alisema Mhandisi Munde.

Aidha, alionesha kuridhishwa na ushirikishwaji wa wataalam katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati. “Jambo ambalo naona ni la kujivunia na kulichukua kwa sisi kama Halmashauri ambao tutatekeleza miradi kama hii kwa baadae ni ushirikishaji wataalam. Hili ni jambo muhimu sana. Unajua kama mradi huufahamu vizuri hata usimamiaji wake unakuwa hafifu” alisisitiza kwa furaha.

Miradi yote tuliyotembelea inaubora unaokubalika na imezingatia thamani ya fedha, aliongeza.

Wakiwa Jijini Dodoma wataalam hao walitembelea ujenzi wa miradi ya kimkakati ya kituo cha kuegesha malori cha Nala, Kiwanda cha kutengeneza matofali-Low cost, kituo kikuu cha mabasi Dodoma na soko kuu la Ndugai.

Kituo Kikuu cha Mabasi ni moja na miradi ya kimkakati ya Jiji la Dodoma kilichotembelewa na timu ya wataalam kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Mhandisi Mshamu Munde.


Eneo la kuegesha malori lililopo Nala ni miongoni mwa miradi ya kimkakati iliyotembelewa na kusifiwa na timu ya wataalam kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.