• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

kongole Rais Dkt. Samia kwa kuin'garisha Dodoma

Imewekwa tarehe: February 13th, 2023

Na. Theresia Nkwanga, DODOMA

Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini, Anthony Mavunde amempongeza Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuing’arisha Dodoma kimiundombinu ikiwa na mtandao mrefu wa barabara za lami na kuchochea maendeleo katika Jiji la Dodoma.

Pongezi hizo alizitoa katika mkutano maalum wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kujadili mapendekezo ya mpango wa Bajeti ya matengenezo ya barabara kwa mwaka wa fedha 2023/2024 katika ukumbi wa mikutano wa Jiji la Dodoma.

Mavunde alisema kuwa Dodoma ni kati ya maeneo ambayo kwa kiwango kikubwa yameguswa na barabara ya lami. Dodoma Jiji inaongoza Tanzania nzima kwa kuwa na mtandao mrefu wa barabara za lami zenye urefu wa Kilometa 194.8 ikifuatiwa na Manispaa ya Kinondoni yenye barabara zenye urefu wa Kilometa 177.

“Tunamshukuru Mheshimiwa Rais kwakutujengea miundombinu ya barabara. Tunaamini kazi hii itaendelea na Dodoma itazidi kupaa na kung’ara zaidi” alisema Mavunde.

Aidha, aliwashauri Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini Wilaya ya Dodoma (TARURA) kujikita zaidi katika kutengeneza kilometa chache za barabara kwa ukamilifu kuliko kufanya matengenezo kwa ukubwa wa kilometa mvua zikinyesha barabara zinaharibika hivyo, kuhitaji matengenezo mengine.

“Kila mwaka tunazitengea fedha lakini zinarudi katika utaratibu uleule kwanini msibadilishe utaratibu badala yakuwa na barabara ya kilometa 10 yenye bajeti ya kilometa 10 kwaajili ya kwenda kukwangua barabara, kwanini msiifanye ikawa kilometa tano, ikatengenezwa kwa ukamilifu ikatumika muda wote mkamalizia kipindi kingine kuliko kutumia fedha ya kilometa 10 kukwangua barabara mvua zikinyesha barabara zinaharibika mnaanza upya” alisema Mavunde.

Naye, Meneja wa TARURA Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Lusako Kilembe, alisema kuwa TARURA katika mwaka wa fedha 2023/2024 imejipanga kutengeneza kilometa 483.4 sawa na asilimia 40 ya kilometa zote za Jiji la Dodoma. Alisema kuwa bajeti hiyo itahusisha matengenezo ya kawaida, ya muda maalumu na maeneo korofi.

“Ukiangalia bajeti yetu kwa haraka kuna takribani kilometa 483.4 zinazoenda kutengenezwa wakati ukiangalia mtandao wetu una kilometa 1,180 zile ambazo zinatambulika na TARURA. Kilometa 696 sawa na asilimia 60 haziguswi kabisa pamoja na kwamba bajeti imeongezeka bado tunachangamoto ukizingatia ukuaji wa kasi wa Jiji la Dodoma. Tunatakiwa kuongeza vyanzo vya mapato ili kuhakikisha mtandao wa barabara tunaweza kuhudumia kwa asilimia kubwa,’’ alisema Mhandisi Kilembe.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.