• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kunambi ashauri makao makuu ya Machinga yajengwe Dodoma

Imewekwa tarehe: July 20th, 2019

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi amelishauri Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania kuhamishia makao yake makuu mjini Dodoma.

Kauli hiyo aliitoa jana alipokuwa akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania kutokana na ushirikiano ambao amekuwa akiwapatia katika kutekeleza majukumu yao jana ofisini kwake.

Kunambi alisema “nataka makao makuu ya Machinga yawe jijini Dodoma. Tutaanza na kutafuta ofisi hapahapa Dodoma”, alisema Kunambi. Vilevile,  aliwashauri kuangalia uwezekano wa kufanya mkutano wa Machinga Tanzania katika Jiji la Dodoma. Mkutano huo ni vizuri ukawa na utoaji wa elimu kuhusiana na masuala mbalimbali kwa Machinga, aliongeza. Katika kuonesha shukrani kwa Rais Dkt. John Magufuli kwa mapenzi yake kwa Machinga, ni vizuri mkamualika kufungua mkutano huo.    

Mkurugenzi wa Jiji aliwataka Machinga kufanya shughuli zao na kukua kimtaji. “Lazima tuwe na mpango wa kufanya mabadiliko kutoka Machinga kwenda kuwa wafanyabiashara. Hata Mbuyu ulianza kama mchicha” alisema Kunambi. Aliushauri umoja huo kuangalia uwezekano kwa kuanzisha vitega uchumi ikiwa ni pamoja na kuwekeza katika hoteli na majengo.

Katika kuhakikisha Machinga wanafanya kazi zao vizuri, Mkurugenzi huyo alisema kuwa Jiji la Dodoma linataka kufanya Machinga wa kisasa. Machinga wanaofanya kazi zao vizuri kwa kuzingatia taratibu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania, Ernest Masanja alisema kuwa umoja huo umeona vizuri kumpa cheti cha shukrani Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutokana na ushirikiano ambao amekuwa akiutoa kwa Machinga katika kutekeleza majukumu yao na jinsi ambavyo amefanikisha zoezi la ugawaji vitambulisho vya wajasilimali. Akiongelea ushauri wa Mkurugenzi wa makao makuu ya Machinga kuhamia Dodoma, alisema wapo tayari. “Kwa kuwa kipenzi chetu Rais, Dkt. John Magufuli anahamia Dodoma na sisi tupo tayari kuhamishia makao makuu ya machinga Dodoma” alisema Masanja.

Jiji la Dodoma ni miongoni mwa Halmashauri ambazo zimemaliza kuuza vitambulisho vyote walivyopewa kwa ajili ya kuwauzia wafanyabiashara wadogo. Vitambulisho 15,173 vya wajasiliamali vimeshauzwa kwa wafanyabiashara kwa bei ya shilingi 20,000 kwa kila kimoja.

Mwenyekiti wa Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania Ernest Masanja akimkabishi cheti Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi ofisini kwake jana.


Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi (katikati) akiwa na viongozi wa Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania walipomtembelea ofisini kwake jana.


Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi akiongea na timu ya uongozi wa Shirika la Umoja wa Machinga waliomtembelea ofisini kwake jana na kujadiliana mambo mbalimbali ya maendeleo. 


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.