• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kwaheri Dkt. Mahenge, karibu Mhe. Mtaka Dodoma

Imewekwa tarehe: May 26th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka amepokea taarifa ya makabidhiano ya Ofisi kutoka kwa Dkt. Binilith Mahenge aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Hafla ya makabidhiano ya Ofisi hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita tarehe 21 Mei, 2021 ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na kuhudhuriwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama, Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Dodoma, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Taasisi zilizopo Mkoani Dodoma, Viongozi wa Dini na wawakilishi wa Wazee wa Mkoa wa Dodoma.

Dkt. Binilith Mahenge amewataka Viongozi Mkoani Dodoma kumpa ushirikiano wa karibu Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka kama walivyofanya kwake.

Akifafanua zaidi, Dkt. Mahenge alisema, mafanikio ya kazi kubwa aliyoifanya akiwa Dodoma yamesababishwa na ushirikiano wa karibu baina yake na viongozi wengine hivyo amewaomba kuendelea kutoa ushirikiano huo kwa Mhe. Mtaka.

"Nawaomba sana viongozi wenzangu, jinsi mlivyonisaidia mimi mfanye hivyo hivyo kwa Mtaka, anawategemea sana katika kutekeleza jukumu la kuleta maendeleo;

Naondoka mimi kama mimi nawaacha, naondoka nikiwa na huzuni kwa sababu nawaacha watu waliokuwa na mimi bega kwa bega, tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa sababu ya ushirikiano," alisema Dkt. Mahenge kwa hisia.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa wa Singida alitumia nafasi hiyo kumtoa wasiwasi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kuwa yupo tayari kushirikiana naye hata kwa kusafiri pale anapohitaji msaada wake.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Anthony Mtaka alimuelezea Dkt. Mahenge kuwa ni kiongozi makini mwenye haiba ya uongozi huku akiahidi kuuenzi uongozi wake na yale aliyoyaacha Dodoma.

“Pamoja na Mahenge kuondoka Dodoma, kamwe hawezi kufanana na baadhi ya viongozi ambao hutumia fursa ya uhamisho wa viongozi wenzao kujitukuza na kuibua upya migogoro iliyokwisha tatuliwa” alisema Mhe. Mtaka.

Aliongeza kuwa hilo tatizo ndilo ambalo limekuwa likichochea migogoro ya ardhi na kusababisha migongano kwenye jamii.

"Kuna migogoro mingi ya ardhi imeshindwa kufikia muafaka kutokana na unafiki wa baadhi ya viongozi, mwenzake akiondoka au kuhamishiwa sehemu nyingine yeye anaanza upya kuibua migogoro ili mwenzake aonekane hakufanya lolote;

Tabia hii ni mbaya, sisi wote ni kitu kimoja tupo kwa ajili ya kuwatumikia Wananchi" alimalizia Mkuu huyo wa Mkoa wa Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.