• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Madiwani wahimizwa kupiga vita lishe duni kwa mtoto

Imewekwa tarehe: June 26th, 2019

MADIWANI wa Halmashauri ya jiji la Dodoma wameshauriwa kukabiliana na athari za lishe duni kwa watoto ili waweze kutoa mchango katika uchumi wa taifa.

Ushauri huo umetolewa na Afisa Lishe wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Semeni Eva Juma alipokuwa akiwasilisha mada juu ya athari za lishe kwa watoto katika mafunzo ya kuwajengea uwezo madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri.

Juma alisema kuwa lishe duni ina madhara makubwa katika makuzi na mustakabali wa maisha ya mtoto. “Athari za lishe duni kwa watoto zinasababisha madhara ya muda mrefu. Madhara hayo ni udumavu wa kimo na kudhoofika kwa mfumo wa kinga ya mwili ambapo hupelekea kuugua mara kwa mara kwa mtoto” alisema Juma. Athari nyingine ni ukuaji wa ubongo na maendeleo ya mtoto kuwa duni jambo linalosababisha uwezo mdogo wa uzalishaji mali wakati wa umri wa utu uzima.

Athari nyingine alizitaja kuwa ni kiribatumbo kwa watoto. “Waheshimiwa madiwani, kiribatumbo kwa watoto kinachangiwa na uzito uliozidi na kisukari cha mimba kwa mama mjamzito husababisha mtoto kuzaliwa na uzito mkubwa. Pia kutokuzingatia taratibu sahihi za unyonyeshaji wa maziwa ya mama” alisema Juma. Athari nyingine ni kutozingatia taratibu sahihi za ulishaji wa chakula cha nyongeza kwa watoto na uelewa duni wa wazazi na walezi kuhusu lishe ya watoto.  

Afisa lishe alizitaja athari nyingine kuwa ni ulaji wa vyakula vyenye nishati lishe kwa wingi na mila na desturi zinazoathiri lishe ya watoto zimekuwa ni changamoto kubwa. Maisha ya mtoto kukaa bila kucheza au kufanya mazoezi kwa muda mrefu huathiri hali ya lishe kwa watoto, aliongeza.

Afisa lishe huyo aliwaelezea madiwani mambo ya kuzingatia katika kupanga mlo kamili kuwa ni kutumia vizuri vyakula vinavyopatikana katika mazingira yanayowazunguka. “Mtoto anatakiwa kula angalau chakula kimoja kutoka katika kila kundi la vyakula. Kiasi cha chakula hutegemeana na umri, jinsia, shughuli na hali ya kifisiologia ya mtoto” alisema Juma. Vilevile, alisisitiza unywaji wa maji safi na salama na kufanya mazoezi mara kwa mara ili kuufanya mwili kuwa na afya bora.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Mbabala, Pascazia Mayalla alisema kuwa mafunzo hayo yamewajengea uwezo madiwani ili waweze kuwa mabalozi wazuri katika uhamasishaji masuala ya lishe katika kata zao. “Napenda kuushukuru uongozi wa halmashauri ya jiji kwa kutuandalia mafunzo hayo. Mafunzo haya yamenifundisha kuchanganya chakula vizuri kwa kuzingatia makundi matano ya vyakula wakati wa kuandaa chakula cha mtoto. Tumekuwa na utaratibu wa kushindilia chakula cha aina moja tu katika mlo wa watoto na sisi wenyewe” alisema Mayalla.

Mayalla alibainisha kuwa wazazi wamekuwa na mchango mkubwa katika udumavu wa watoto. “Watoto tunawaambia mjinga wewe kumbe mzazi ndiye umechangia tatizo hilo. Mama anatakiwa kumuandaa mtoto toka akiwa tumboni kwa mama yake. Udumavu unasababishwa na sisi wazazi si watoto. Wazazi ndiyo tunatakiwa kuwaandaa watoto wetu kwa kuwapa lishe bora” alisisitiza Mayalla.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.