• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maadhimisho wiki ya Huduma za Fedha kuinua Uchumi jumuishi

Imewekwa tarehe: November 17th, 2022

SERIKALI imejipanga kuhakikisha wananchi wengi wanapata uelewa wa masuala ya fedha ili kuwawezesha kushiriki katika uchumi jumuishi na kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi.

Hayo yameelezwa jijini Dodoma na Kamishna wa Idara ya Maendeleo ya Sekta ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Charles Mwamwaja alipokutana na wanahabari kuzungumzia Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa inatarajiwa kufanyika mkoani Mwanza kuanzia Novemba 21 hadi 26, 2022 yenye kauli mbiu “Elimu ya Fedha kwa Maendeleo ya Watu”.

Dkt. Mwamwaja alisema Serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kutoa elimu kwa umma kuhusu masula ya fedha ikiwemo maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa ili kutimiza lengo la Serikali la kuhakikishasha takriban asilimia 80 ya wananchi wanapata uelewa wa masuala ya fedha ifikapo mwaka 2025.

“Kutokana na Utafiti wa FinScope wa mwaka 2017 nchini, ni asilimia 48.6 tu ya nguvu kazi ndiyo waliotumia huduma rasmi za fedha na hivyo kubaki na kundi kubwa la Watanzania ambao hawafaidiki na huduma hizo na hivyo kukosa fursa za kuboresha maisha yao kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi na hatimaye kuchangia katika kukuza Pato la Taifa”, alifafanua Dkt. Mwamwaja.

Alisema Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imelenga kutumia maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa ili kujenga uelewa na weledi kwa umma katika matumizi sahihi ya huduma za fedha zinazotolewa, kujenga uchumi na kuondoa umaskini pamoja na kuongeza upatikanaji wa huduma za fedha.

Dkt. Mwamwaja alisema wamelenga pia kutoa elimu ya kuwezesha kumlinda mtumiaji wa huduma za fedha, kuwezesha wananchi kusimamia vizuri rasilimali fedha na kuwezesha wajasiriamali wadogo kuongeza ujuzi na matumizi sahihi ya huduma za fedha katika kukuza biashara zao.

“Tunalenga kuimarisha ufanisi wa masoko ya fedha kupitia elimu ya fedha, kuongeza upatikanaji wa huduma za fedha, kuimarika kwa utamaduni wa kujiwekea akiba, kukopa na kulipa madeni”, alibainisha Dkt. Mwamwaja.

Alisema katika kufanikisha hilo Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango itashirikiana na wadau wengine wa masuala ya fedha zikiwemo wizara, idara, Wakala wa Serikali, wasimamizi wa Sekta ya Fedha, Taasisi za Fedha, Asasi zisizo za kiserikali, Sekta Binafsi, Bodi za Wataalamu, Vyama vya Wafanyakazi, Vyombo vya Habari, Taasisi za Elimu na Utafiti, Washirika wa Maendeleo, Vyama vilele vya Sekta ya Fedha, Makundi ya Watoaji huduma za fedha na Taasisi za Dini zinazotoa huduma hizo.

Aidha, alitoa wito kwa wananchi wote hususani wale wanaoishi Kanda ya Ziwa kushiriki maonesho hayo kikamilifu ili kuweza kupata elimu hiyo muhimu katika kukuza uchumi wao na wa Taifa kwa ujumla.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.