• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maafisa Kilimo Jiji wapewa mafunzo ya kilimo cha zabibu

Imewekwa tarehe: August 4th, 2021

Na. Sifa Stanley, DODOMA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kushirikiana na taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania tawi la Makutupora (Tanzania Agriculture Research Institute- TARI) wametoa mafunzo ya kilimo cha zao la Zabibu kwa maafisa kilimo wa kata za Jiji la Dodoma ikiwa ni utekelezaji wa agizo la waziri mkuu.

Mafunzo hayo yalitolewa tarehe 4 Agosti, 2021, eneo la Nanenane katika Kata ya Nzuguni, Jijini Dodoma.

Akiongelea mafunzo hayo, Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Agnes Woisso alisema kuwa mafunzo hayo yamefanyika kufuatia agizo la Waziri Mkuu wa Tanzania tarehe 6 Julai, 2021 alipotembelea na kukagua shughuli katika kituo cha utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Makutupora. Alisema kuwa waziri mkuu aliagiza yatolewe mafunzo ya kilimo cha zao la Zabibu kwa maafisa kilimo wote wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Katika mafunzo hayo, Mtafiti wa Kilimo kutoka TARI tawi la Makutopora, Dainess Sanga alielezea namna nzuri ya kuandaa shamba la zabibu, uchaguzi mzuri wa mbegu, uandaaji wa mbegu, pamoja na uandaaji wa mbolea na matumizi sahihi ya mbolea. Vilevile, alielezea aina mbalimbali ya Zabibu pamoja na matumizi yake. “Ni muhimu kuzingatia aina bora ya mbegu na kufanya maandalizi mazuri ya upandaji wa mbegu ili kupata mavuno mazuri” alisema Sanga.

Kwa upande mwingine Prosper Rema, ambaye ni afisa kilimo kutoka TARI tawi la Makutupora alitoa mafunzo ya namna bora ya ukataji wa mbegu za Zabibu na dawa bora za zao hilo Pamoja na njia bora ya upigaji dawa wa zao la Zabibu. Aidha, aliwafundisha maafisa kilimo wa halmashauri jinsi ya kuhudumia mmea wa zao la Zabibu ambapo mafunzo hayo aliyafanya kwa vitendo katika vitaru vya zao la Zabibu.  

“Huduma nzuri ya mmea huchangia ukuaji mzuri wa mmea na mazao huwa ya kuridhisha. Hivyo, ni vema kuzingatia huduma kwa mmea” alieleza Rema.

Akiongelea umuhimu wa mafunzo hayo, Afisa Kilimo kutoka Kata ya Ihumwa, Swaiba Msangi alisema kuwa mafunzo hayo yamewapa ujuzi wa njia bora ya kulima zao la Zabibu. “Mafunzo haya yamenisaidia kupata ujuzi wa namna bora ya kufanya kilimo cha zao la Zabibu. Mafunzo haya yataimarisha kilimo hicho katika Jiji la Dodoma” alisema Msangi.

Aidha, ameiomba serikali kuimarisha masoko ya zao la Zabibu kwa kuhamasisha wawekezaji zaidi kununua zao hilo kutokana na soko la ndani na nje ya nchi kuwa changamoto.

Mafunzo hayo endelevu yalihudhuriwa na Maafisa kilimo kumi na saba wa ngazi za kata, watafiti wa kilimo kutoka Taasisi ya Utafiti wa kilimo, tawi la Makutupora.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.