• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maafisa Maendeleo ya Jamii waonywa utoaji Mikopo

Imewekwa tarehe: November 10th, 2022

SERIKALI imewataka Maafisa Maendeleo nchini kuacha kutumia vyeo vyao kwa kuweka taarifa hewa za vikundi vya mikopo ya asilimia 10 kwa lengo la kujinufaisha.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Angellah Kairuki wakati akifunga kikao kazi cha Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka Sekretarieti za Mikoa na Wakuu wa Idara wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini, uliofanyika Jijini Dodoma, kuanzia tarehe 8 hadi 10 Novemba, 2022, katika Ukumbi wa hoteli ya Morena.

Kairuki amewaonya vikali Maafisa hao wanaotumia vibaya vyeo vyao wajilekebishe mara moja vinginevyo watakutana na mkono wa Dola kwa mujibu wa Sheria zilizowekwa.

"Naomba kama wapo ambao huko nyuma kabla ya leo tarehe 10, walikuwa na makandokando hayo tubadilike, ni tamaa ambazo hazina baraka na ni wizi wa kuwaibia walipa kodi na wanasononeka, machozi yao hata siku moja hayatakufikisha sehemu salama" amesema Kairuki.

Kairuki amesema hatarajii kuona kesi baada ya tarehe ya leo, wala kusikia kesi za Manispaa mbalimbali kama vile Manispaa ya Ilala, Kinondoni na Kalambo kuanza kupokea kesi wakati maelekezo yalikwishatolewa na Katibu Mkuu wakati wa kikao kazi.

Aidha, amezitaka Halmashauri nchini kuendelea kutumia Mfumo wa kieletroniki wa mapato ya Asilimia 10 ili kuhakikisha kuwa Mikopo yote iliyotolewa na inayoendelea kutolewa inaratibiwa, kukusanywa kama madeni na kurejeshwa kwa wakati ili wengine wanufaike na mikopo hiyo.

"Naomba nisisitize fedha hizi ni mikopo inayotakiwa kurejeshwa na kuweza kuwakopesha wahitaji wengine, Halmashauri zote zihakikishe zinaweka Mikakati ya kukusanya madeni hayo na ifikapo mwezi Februari, 2023 nusu ya madeni hayo ambayo
yamepitwa na muda yawe yamerejeshwa na hatua sitahiki ziwe zimechukuliwa kulingana na Kanuni zilizopo” amesema Kairuki.

Akimkaribisha mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula amewaasa Maafisa hao kufanya kazi kwa moyo, juhudi ni
maarifa lakini pia kutimiza wajibu wao kwenye maeneo yao ya kazi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.