• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maafisa Mawasiliano waaswa kutoa taarifa za kimkakati

Imewekwa tarehe: September 20th, 2019

Serikali imewataka Maafisa Mawasiliano, Habari na Uhusiano kutumia ujuzi na weledi wao kuisemea, kuitangaza mipango na mikakati ya Serikali kwa haraka, ukweli na uhakika kimkakati ili ujumbe huo uwafikie walengwa kwa wakati.

Rai hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamhanga wakati akifunga mafunzo ya siku tano kwa Wasemaji wa Serikali toka Wizara, Taasisi za Serikali, Wakala mbalimbali za Serikali, Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Halmashauri za Wilaya katika ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma leo.

“kwa mafunzo haya mliyoyapata, ninyi mkiwa kama Wasemaji wa Serikali katika maeneo yenu ya kazi, mtaweza kuhabarisha wananchi kuhusu miradi na utekelezaji wa mipango na mikakati ya Serikali”. Alisema Mhandisi Nyamhanga.

Amesema ni muhimu sasa kuwa na mafunzo ya mara kwa mara na endelevu ili kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia katika kuhabarisha Umma masuala ya kimaendeleo na kiuchumi kwa jamii

“ni muhimu sana kuwa na mafunzo ya mara kwa mara ambayo yanawaongezeeni ujuzi ili muweze kwenda na wakati katika kufikisha habari kwa walengwa, mwendelezo wa kujinoa katika kufikisha habari na taarifa sahihi kwa wakati”

Aidha, amesema Mafunzo ya mawasiliano ya kimkakati ni muhimu sana hasa wakati huu ambapo Serikali ya Awamu ya Tano inafanya mageuzi makubwa ya kiuchumi kama vile Mradi Mkubwa wa Kufua Umeme (Julius Nyerere Hydro-Power Project) wa Megawati 2115, Ujenzi wa vituo vya afya 352, hospitali za wilaya 67 na 27 katika mwaka 2019/2020 na zahanati, miundombinu ya barabara, madaraja, viwanja vya ndege, na utoaji wa Elimu Bila Malipo ambao kwa 2019/2020 shilingi 288.485 zimetengwa.

Mageuzi mengine ni pamoja na sheria mpya ya mapato ambapo mapato ya madini pekee yanatarajiwa kufikia shilingi Bilioni 420 mwaka 2019/2020, ununuzi wa ndege mpya na ujenzi wa treni ya umeme ya kisasa (Standard Gauge Railway) kutoka Dar es Salaam – Morogoro shilingi trilioni saba.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Bw. Jonas Kamaleki amesema mafunzo hayo ya siku tano yanalenga kuwajengea uwezo Maafisa hao ili waweze kutoa taarifa kwa usahihi, umakini na wakati, kutoa taarifa kimkakati, kutoa taarifa kwa Umma kwa mpangilio wa kisasa, usahihi na weledi.

Naye Bi. Sarah Kibonde   Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) amesema katika mafunzo hayo jumla ya washiriki 141 wamehudhuria na yamelenga zaidi kuwajengea uwezo Maafisa hao ili wawee kufanya kazi zao kwa weledi.

Akiongea kwa niaba ya washiriki, Benton Nollo Afisa Habari kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma amesema ofisi za Maafisa hao hasa katika Mikoa na Halmashauri nchini wanakabiliwa na uhaba wa vifaa, bajeti ndogo, kutotakumbulika kwa Vitengo vya Habari na kutoshirikishwa kwenye baadhi ya miradi ya Maendeleo kwenye maeneo yao.

Mafunzo hayo ya siku tano yameandaliwa chini ya Idara ya Habari Maelezo na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) ambapo Maafisa na Wasemaji hao walijifunza kuhusu uandikaji wa habari kwa weledi, taarifa kwa Umma (Press Release), kuandaa vipindi bora vya televisheni na utumiaji wa mitandao ya kijamii.

Chanzo: Tovuti ya tamisemi.go.tz


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.