• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

'Msako' mkali wezi wa Mchanga

Imewekwa tarehe: October 11th, 2018

Katika kutekeleza agizo la Makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan, juu ya kutunza mazingira, wataalam wa mazingira kutoka jiji la Dodoma kwa kushirikiana na viongozi wa kata ya Ntyuka, leo wamefanya operesheni ya kukagua stakabadhi za malipo ya vifusi vya mchanga kwenye vifanda vya tofali vilivyopo kata hiyo ili kubaini watu wanaochimba mchanga na kusafirisha usiku katika eneo la mtaa wa Chidachi lililozuiliwa kwa mujibu wa sheria za mazingira.

Mkuu wa Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu Jiji la Dodoma Dickson Kimaro amesema, kutokana na baadhi ya watu wanaomiliki viwanda kula njama na wamiliki wa malori kusafirisha mchanga na kuumwaga nyakati za usiku, opereshani hizi zitafanyika mara kwa mara kwa lengo la kukagua stakabadhi za ununuzi wa mchanga kutoka kwa wamiliki wa malori ya kubebea mchanga.

Kimaro ameagiza wafanyabiashara wote wenye viwanda vya tofari na wananchi wanaofanya ujenzi wahakikishe wanachimba mchanga maeneo yaliyoruhusiwa ambayo ni Zuzu, Mtumba, Ihumwa, Iyumbu na Mpunguzi. Watu wote wahakikishe wanapatiwa stakabadhi halali, la sivyo watatafsiriwa kuwa wezi na hatua stahiki zitachukuliwa dhidi yao ikiwa ni pamoja na kuwapeleka mahakamani.

Diwani wa kata ya Ntyuka Mheshimiwa Teobart Maina amesema zaidi ya hekta 20 zimeharibiwa vibaya na wachimbaji wa mchanga likiwemo eneo la Ukanda wa Kijani. Kwa kutambua umuhimu wa eneo hilo Maina amesema doria za mara kwa mara zitaendelea kufanyika ili kuwadhibiti wezi wa madini ujenzi hasa nyakati za usiku.

Afisa Mtendaji wa kata ya Ntyuka Vestina Manota amewaagiza wamiliki wa viwanda vya tofali kuhakikisha wanachukua taarifa za watu wanaowauzia mchanga kwa kuandika jina la dereva, namba ya simu, namba ya gari linalobeba mchanga na nakala ya stakabadhi za malipo ya ushuru.

Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Chidachi Merina Nzunda amesema wataendelea kufanya doria katika eneo hilo kila siku na kupita katika viwanda vya tofari ili kukagua stakabadhi na taarifa zote zitapelekwa kwa Mtendaji wa kata.

Jitihada hizi za Halmashauri ya Jiji la Dodoma zina lengo la kuhakikisha kasi ya ujenzi katika jiji la Dodoma inaenda sambamba na utunzaji wa mazingira.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.