• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maafisa Ugani Jiji 'fasta' wakabidhiwa pikipiki zao

Imewekwa tarehe: June 8th, 2022

Na. Shaban Ally, DODOMA. 

NAIBU MEYA wa Jiji la Dodoma, Mhe. Emmanuel Chibago ameongoza zoezi la kukabidhi pikipiki kwa Maafisa Ugani wa Halmashauri ya jiji la Dodoma ili kuboresha huduma ya kilimo kwa wakulima ndani ya halmashauri hiyo.

Zoezi hilo limefanyika kwenye ofisi za Idara ya Kilimo ambapo Chibago alikabidhi takribani pikipiki 25 kwa maafisa Ugani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ili kuongeza ufanisi kwenye majukumu yao lakini pia Chibago hakusita kutoa pongezi kwa Rais, Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia maafisa Kilimo pikipiki ili kurahisisha utendaji wao wa kazi. Aidha makabidhiano hayo yamefanyika kutekeleza agizo la Waziri Mkuu alilolitoa kwa Wizara ya Kilimo kuhakikisha pikipiki hizo ziwafafikia walengwa katika kipindi cha siku tano kuanzia leo tarehe 8 Juni, 2022.

"Tunaomba tutoe pongezi kubwa kwa Rais wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hassan kwa hiki alichokifanya kwa kutoa vyombo hivi vya usafiri kwa maafisa wetu wa Kilimo, kitendo cha Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kugawa vitendea kazi kwa maafisa ugani tuliowaamini kufanya kazi hii, kinafungua ukurasa mpya wa muendelezo wa Kilimo chetu”, alisema Chibago.

Kwa upande mwingine Mkuu wa idara ya Kilimo, Yustina Munishi akielezea malengo ya Wizara ya Kilimo mpaka kufikia mwaka 2030, alisema "Tunakabidhi pikipiki takribani 25 kwa lengo la kutekeleza ajenda ya kilimo kufikia 2030 mchango wa Kilimo kwenye uchumi wa nchi uongezeke kwa 10%".

Yustina aliongeza kuwa maafisa Kilimo wamepewa pikipiki hizo kwa lengo la kuwezesha kutekeleza ajenda zilizowekwa na wizara ya kilimo ambapo ni kutoa huduma bora za ugani, kuongeza mnyororo wa thamani wa mazao pamoja na kutoa elimu bora kwa wakulima.

Sambamba na hilo, Chibago aliwaasa maafisa ugani waliokabidhiwa pikipiki hizo kuzitumia kwa shughuli za Kilimo tu na si vinginevyo, "Kupitia makabidhiano haya niwaase ndugu zetu maafisa ugani ambao mmekabidhiwa vifaa hivi kuwa vitumike kwa kuhudumia wakulima na si kubebea mkaa".




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.