• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maafisa wa Serikali ya Nigeria waanza ziara Tanzania kujifunza shughuli za TASAF

Imewekwa tarehe: September 19th, 2020

UJUMBE wa Maafisa wa Serikali ya Nigeria wapatao 33 umeanza ziara ya siku Nane nchini kujifunza namna Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF unavyotekeleza majukumu yake kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini-PSSN.

Akiwakaribisha Maafisa hao, Mkurugenzi wa Miradi wa TASAF, Bwana Amadeus Kamagenge amesema Mkakati wa Serikali ya Tanzania kupambana na umaskini kupitia TASAF umekuwa na mafanikio makubwa na umeamsha ari ya wananchi kuboresha maisha yao.

Bwana Kamagenge amesema mkazo mkubwa umewekwa katika uhamasishaji wa Walengwa kushiriki kwenye kazi za uzalishaji mali huku sekta ya elimu na afya hususani kwa watoto kutoka katika kaya za Walengwa zikipewa msukumo mkubwa zaidi kwenye shughuli za Mpango.

Aidha Mkurugenzi huyo wa Miradi wa TASAF amesema mafanikio yaliyopatikana tangu kuanza kwa shughuli za Mpango yamechangiwa kwa kiwango kikubwa na ushiriki wa Walengwa na Mchango mkubwa wa Serikali na Wadau mbalimbali wa Maendeleo.

Kwa upande wao Maafisa hao kutoka nchini Nigeria wamesema uamuzi wa kuja Tanzania kujifunza umetokana na taarifa walizonazo juu ya mafanikio makubwa ambayo Serikali ya Tanzania kupitia TASAF imepata kwa kuzifikia Kaya za Walengwa na kuzihudumia kwa mafanikio makubwa katika kupunguza kero ya umaskini kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ambao ni wa aina yake kupata kutekelezwa barani Afrika.

Ujumbe huo wa Maafisa kutoka Nigeria, mbali na kupata maelezo ya shughuli za TASAF katika Ofisi ndogo za Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam pia utapata fursa ya kutembelea Unguja ambako utakutana na Maafisa wa Serikali na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kisiwani humo. Hii ni mara ya Pili kwa Maafisa wa serikali kutoka Nigeria kutembelea Tanzania kujifunza namna TASAF inavyotekeleza majukumu yake kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini.

Chanzo: Blog ya TASAF

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.