• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maafisa Waandikishaji waaswa uadilifu

Imewekwa tarehe: October 12th, 2024

Na. Faraja Mbise, DODOMA

Maafisa waandikishaji orodha ya wapiga kura uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameaswa kuwa waadilifu ili Dodoma iwe ya Kwanza kwa idadi kubwa ya watu walioandikishwa.

Hayo yalisemwa na Mjumbe wa Kamati ya Uratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma, ColethaKiwale wakati akizungumza na maafisa waandikishaji, watendaji wa mitaa, wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata pamoja na maafisa watendaji wa kata wakati wa mafunzo kwa maafisa waandikishaji wa orodha ya wapiga kura leo katika ukumbi wa Mtumba Complex jijini Dodoma.

Kiwale aliwataka maafisa waandikishaji kuwa weledi na wenye ufanisi katika suala la muda, mavazi na utoaji taarifa kwa wakati. Msisitizo mwingine alisisitiza wawe waadilifu na wahamasishaji kwa waandikishaji kujitokeza

kwa wingi katika kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura.

“Napenda tushirikishane tunapoelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, tungependa kuwaambia mambo ya kuzingatia mambo yafuatayo: moja, muda wa kufungua vituo na kufunga vituo. Pili, Tunawaomba maafisa

uandikishaji kuwa wahamasishaji wa watu kuja kujiandikisha, pamoja na familia zao kwasababu Mkuu wa Mkoa wa Dodoma anatamani Dodoma iongoze kwa idadi kubwa ya watu watakaokuwa wamejiandikisha kwenye orodha ya daftari nchi nzima, kutoa taarifa za uandikishaji mpaka inapofika saa moja na nusu jioni kwa kufuata muundo wa kitaasisi. Maafisa waandikishaji kuripoti kwa Afisa Mtendaji wa Mtaa. Pia hatutarajii Afisa Mwandikishaji kutafutwa kwenye simu na asipatikane” alisisitiza Kiwale.

Kwa upande wake CPA. Eric Ntikahera, aliwataka maafisa waandikishaji kufanya mambo muhimu tu yanayohusu zoezi la uandikishaji. Aliwataka wafuate maadili na kanuni za utumishi na uadilifu pindi wawapo katika vituo vya

kujiandikisha. Vilevile, aliwataka wasigeuze vituo hivyo kama sehemu ya starehe bali waheshimu vituo hivyo vya kuandikishia kama wanavyoheshimu sehemu nyingine za kazi.

“Mwaka 2019 tulifundisha maafisa waandikishaji wakaelewa, lakini nafikiri ilikuwa vitu viwili tofauti, mtu kapewa elfu kumi yake ya chakula yeye kanunua bia nne pembeni, yaani uandikishaji unaendelea na ulevi

unaendelea. Kwahiyo, kimsingi tijiepushe katika vitu vitakavyokwamisha hili zoezi” alisema CPA. Ntikahera.

Wakati huohuo, Afisa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Albert Kasoga alipokea salamu hizo kutoka Ofisiya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na kuahidi utekelezaji katika zoezi la uandikishaji orodha wa wapiga kura kwa

weledi. “Tunamuahidi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kutekeleza yale aliyoagiza ili Dodoma iwe ya kwanza katika zoezi la uandikishaji kwenye orodha ya wapiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchi nzima” alisema Kasoga.

Ikumbukwe kuwa zoezi hilo la uandikishaji wa orodha ya wapiga kura halitahusisha uwepo wa kadi au kitambulisho  cha mpiga kura, ilimradi tu mwananchi awe amejiandikisha katika orodha ya wapiga kura, vitambulisho vitakavyohusika ni leseni ya udereva, kadi ya Bima ya Afya, kitambulisho cha kazi au kitambulisho cha Taifa (NIDA). Iwapo mwananchi hana atatambulishwa na jirani yake wa mtaa husika.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.