• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maboresho makubwa sekta ya Afya Dodoma

Imewekwa tarehe: March 23rd, 2023

Na. Dennis Gondwe na Theresia Nkwanga, DODOMA

AFYA bora ni nguzo muhimu sana Katika kuhakikisha wananchi wana ukamilifu wa mwili, akili na kuepuka maradhi.Katika kipindi cha miaka miwili kumekuwa na kuongezeka kwa idadi ya vituo vya kutolea huduma za afya.

Serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imejipambanua katika kuboresha huduma za Afya katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ikiongeza vituo vya kutoa huduma za Afya kufikia 116.

Maendeleo ya taifa ni mchakato unaoanzia katika maendeleo ya mtu mmoja mmoja, familia, jamii hadi ngazi ya taifa. Ili dhana ya maendeleo iwe halisia na yenye maana suala la wananchi kuwa na afya njema haliwezi kupingika. Katika kuamini kwenye dhana hiyo miaka miwili ya serikali ya awamu ya sita imejielekeza katika kuboresha sekta ya afya ili wakazi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Makao Makuu ya nchi wawe na afya bora.

Mkuu wa Divisheni ya Afya, Utawi wa Jamii na Lishe katikaHalmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method anasema katika miaka miwili ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan vituo vya kutolea huduma za Afya vimeongezeka kutoka vituo 100 mwaka 2020 hadi kufikia vituo 116 mwaka 2023. Kati ya vituo hivyo,Hospitali zipo saba, kati ya hizo hospitali mbili ni za serikali, Mashirika ya dini hospitali mbili,Mashirika ya Umma hospitali mbili, na watu binafsi Hospitali moja. Vituo vya Afya ni 12, kati ya hivyo, vituo vitano ni vya serikali, kimoja ni cha shirika la dini, vituo vitatu ni vya mashirika ya umma na vituo vitatu ni vya watu binafsi.

Ongezeko hilo linatajwa pia katika Zahanati. Zahanati zipo 81 ambazo zimegawanyika kama ifuatavyo; zahanati za serikali 37, mashirika ya dini 11,mashirika ya umma tisa, zahanati zawatu binafisi 24. Kuna jumla ya kliniki maalumu 14 zinazomilikiwa na watu binafsi. Kituo cha uchunguzi kimoja(Diagnostic center) na maternity home moja anasema Dkt. Method.

Ongezeko la vituo vya kutolea huduma za afya limeenda sambamba na ongezeko la watumishi wa sekta ya Afya katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, katika kipindi cha miaka miwili ya serikali ya awamu ya sita watumishi wameongezeka kutoka watumishi 472 hadi kufikia watumishi 509.

Ongezeko hilo linatokana na Halmashauri kupata watumishi wapya 37 wa sekta ya Afya sawa na ongezeko la asilimia nne ya watumishi wanaohitajika. Watumishi hao wamepangwa katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma ili kuboresha utoaji wa huduma za afya katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Ama kwa hakika hakuna kama Mama, Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan inaendelea kutoa kipaumbele kwenye huduma za afya kwa kuboresha huduma na kuhakikisha zinawafikia wananchi wote alisisitiza Daktari Andrew


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.