• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Machifu wamkaribisha DC Dodoma, wamshukuru Rais kwa chanjo

Imewekwa tarehe: August 6th, 2021

Na Getruda Shomi, DODOMA

MACHIFU wa Mkoa wa Dodoma wakiongozwa na Chifu Mkuu wa Kanda ya Kati Mazengo II, wamemkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Jabir Shekimweri baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kumteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma.

Wametoa tamko la kumkaribisha Mkuu huyo wa Wilaya katika hafla iliyofanyika leo Agosti 6, 2021 katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ambapo walikutana na Mkuu huyo wa Wilaya.

Akiongoza hafla hiyo, Chifu Mazengo II alimkabidhi Mhe. Shekimweri kiti cha miguu mitatu na shuka ikiwa ni ishara ya upendo, amani na ushirikiano.

Mkuu huyo wa Wilaya ya Dodoma alipewa jina la Bilinje na Machifu hao ikiwa ni kumkaribisha na kumpa utawala wa Kichifu katika Wilaya ya Dodoma na kuwa ni mshauri wa Baraza la Machifu.

“Sisi ni Wagogo na wewe tunakukaribisha katika Ugogo, kwa maana hiyo tunakuomba uwe mshauri katika Baraza la Machifu”.

Hata hivyo, risala ya Machifu hao iliyosomwa na Katibu Msaidizi wa Machifu, Chifu Ally Issa Bilinje wa Dodoma Makulu ndugu Jackson Ligoha iliezea changamoto za Machifu ikiwemo, kukosa ofisi, usafiri, semina kwa Machifu, lakini pia risala hiyo ilimuomba Mkuu huyo wa Wilaya kuanzisha sehemu ya Makumbusho kwa ajili ya utalii ikiwemo Maliteli, uhunzi na Ufinyanzi ili kuhamasisha watu kujifunza historia ya Jiji la Dodoma.

Katika hafla hiyo Chifu Mazengo II aliainisha kazi zinazofanywa na Machifu hao kuwa ni pamoja na kuhimiza maendeleo ya nchi, kukemea mambo maovu yanayotendeka katika jamii, na kurudisha mahusiano mema katika sehemu zisizo na maelewano.

Aidha, aliwaomba Machifu wenzake wawe mabalozi katika jamii zao kuhimiza watu kupata chanjo ya UVIKO-19 inayotolewa katika vituo vya afya elekezi Jijini humo.

”Ndugu Machifu na wajumbe wote mliofika, sasa hivi tuna gonjwa hili la Corona, tunamshukuru Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameliona hilo na ametuletea chanjo, basi sisi tuwe mabalozi, tuhamasishe watu wajitokeze kwa ajili ya chanjo” alisema.

Aliongeza kuwa gonjwa hilo linaua hivyo kila Chief ahimize wakazi wa eneo lake kupata chanjo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.