• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Machinga kwenye 'mjengo' wa bilioni 7.5 jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: December 21st, 2021

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imesaini mkataba na kampuni ya Mohamed Builders Limited wa ujenzi wa awamu ya kwanza Jengo la kisasa la wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga Open Market) kwa thamani ya shilingi Bilioni 4.95 kwa ujenzi wa awamu ya kwanza, ambapo hadi kukamilika mradi huo utagharimu shilingi bilioni 7.5 fedha kutoka katika mapato ya ndani na zingine kutoka serikali kuu

Mradi huo unatekelezwa eneo la Bahi Road Jijini humo na utachukua eneo la mita za mraba 14,235 ambapo ujenzi wa mradi kwa awamu ya kwanza utatekelezwa kwa muda wa miezi minne yaani siku 120.

Akitoa taarifa  ya utekelezaji wa mradi huo, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru alisema kujengwa kwa mradi huo kutakuwa na faida nyingi kwa wafanya biashara na Taifa kwa ujumla ikiwemo ukusanyaji wa mapato, kuliweka jiji la Dodoma katika mandhari safi, pamoja na kurahisisha shughuli za usafi na utunzaji wa mazingira.

Mafuru alisema wafanyabiashara ndogo  wapatao 2,938 watakuwa na ajira ya uhakika kwa kufanya biashara katika eneo maalum linalotambulika na kurahisisha utoaji wa huduma za msingi kwa wafanyabiashara hao kama huduma za vyoo, huduma za kifedha, na ulinzi wa mali zao.

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa,  kujengwa kwa mradi huu kutakuwa na faida nyingi kwa Jiji la Dodoma, wafanyabiashara, na Taifa kwa ujumla  hapa naelezea baadhi ya faida hizo kuwa ni Pamoja na ukusanyaji wa mapato, kuliweka Jiji la Dodoma katika mandhari safi, kurahisisha shughuli za usafi na utunzaji wa mazingira” alisema Mkurugenzi huyo.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa, Anthony Mtaka  akiwa mgeni rasmi katika tukio hilo alisema kuwa kukamilika kwa jengo hilo ni ukombozi na hatua kubwa kwa wafanyabiashara hao ambapo watahamia kwa hiari yao katika eneo hilo na kutoka katika maeneo yasiyo tambulika kisheria.

Mkuu huyo wa Mkoa alikemea tabia ya baadhi ya wafanyabiashara ndogo  kujisajili kwa majina ya udanganyifu huku ikiwa ni mbinu ya kuwasajilia watu wasio walengwa katika mradi ambapo alisema watakaobainika kufanya vitendo hivyo watachukuliwa hatua za kinidhamu.

“Mkurugenzi tukishakamilisha ujenzi wa eneo hili hatutarajii kuona kuna Machinga yeyote atakayeshindwa kuhamia katika eneo linalotambulika kisheria,  matarajio yangu ni kwamba viongozi wa wafanyabiashara hawa watatusaidia katika kusimamia hilo” alisema.

“Naomba kukemea baadhi ya tabia zilizoibuka kwa baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu kujiorodhesha kwa majina ya udanganyifu kwa lengo la kuwashikia maeneo watu wasio walengwa wa mradi huu, tukikubaini katika vitendo hivyo hautaruhusiwa kufanya biashara katika eneo hili, tutakutoa mara moja ” alisisitiza Mkuu wa Mkoa  Mtaka.

Naye Mwenyekiti wa wafanyabiashara wadogo Bruno Mponzi alisema wafanyabiashara hao wamepata matumaini makubwa ya kukua kibiashara kwa kupata eneo hilo kwani kutasaidia wao kukuza mitaji na kukatatua kero walizokuwa wakikutana nazo katika maeneo yasiyo rasmi .

“Viongozi wakuu wote,  kwa niaba ya machinga wote tunaona faraja na tunajivunia uongozi wenu,  kwani kwa  eneo hili lenye ukubwa wa kutosha tuna matumaini sasa tunakwenda kukuza mitaji yetu na uwepo wa eneo hili sasa unatatua ile changamoto na adha tulizokuwa tunakutanana nazo katika maeneo yasiyo rasimi” alisema Mponzi.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Mohamed Builders Limited, Taher Mustafa  alisema watatekeleza mradi kwa muda sahihi kwa mujibu wa mkataba ambao ni miezi minne.

“Kampuni yetu ya Mohamed Builders Limited imetekeleza miradi mingi ya Serikali hivyo tunashukuru kwa kupata tena nafasi nyingine ya kutekeleza mradi huu, sisi kama kampuni tutajitahidi kukamilisha mradi huu ndani ya muda husika kama ilivyo katika makubaliano ya mkataba wetu” alisema Mustafa.

Mkuu wa mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka aliyekuwa mgeni rasmi wa utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa eneo maalum la wafanyabiashara wadogo 'Machinga' Jijini Dodoma katika eneo la Bahi Road. 

 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Joseph Mafuru.

Baadhi ya wananchi na wafanyabiashara wadogo 'machinga' waliohudhuria utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa eneo la machinga.

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Mohamed Builders Limited, Taher Mustafa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.