• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Machinga Nyerere Square waonywa

Imewekwa tarehe: March 18th, 2020

Halmashauri ya Jiji la Dodmoa, imetoa onyo kwa wafanyabiashara wadogo (Machinga) kuacha kupanga bidhaa zao kabla ya muda uliopangwa kwenye barabara pembeni ya Nyerere Square inayotumika kama 'soko la jioni' ili kutozuia watumiaji wengine wa barabara.

Katika barabara hiyo, wafanyabiashara hao wanapaswa kupanga bidhaa zao kuanzia saa 10:00 jioni baada ya muda wa kazi kuisha, lakini wameonekana kukiuka utaratibu huo na kuanza kupanga kabla ya muda huo.

Onyo hilo lilitolewa jana na Ofisa Masoko wa Jiji la Dodoma, James Yuna, alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara hao wanaofanya biashara katika eneo hilo.

Alisema hivi sasa wamekuwa wakipanga bidhaa muda wa asubuhi hali inayoleta usumbufu kwa watumiaji wengine wa barabara.

“Wafanyabiashara mnapaswa kufuata sheria, kanuni na maagizo yaliyoelekezwa na jiji ya kufanya biashara zao kwa muda waliopangiwa ili barabara hii itumike kwa shughuli nyingine,” alisema.

Aliongeza: “Jiji halitakuwa tayari kuwaona baadhi yenu mkikiuka maelekezo mliyopewa ya kufanya biashara zenu kwa muda mlioambiwa wa kuanzia saa kumi hadi saa tatu usiku, vinginevyo tutawaondoa bila nyinyi kupenda suala ambalo halina tija kwa pande zote hivyo ninawataka mzingatie maelekezo na si vinginevyo.”

Sambamba na hilo, aliwataka kuzingatia usafi kwenye maeneo ambayo wamekuwa wakifanya biashara zao.

“Hii ni pamoja na kutokiuka maelekezo ya maeneo mnayotakiwa kufanya shughuli zenu ili kuepukana kuondolewa kwa nguvu na kusababisha hasara ya bidhaa zenu,” alisema.

Kadhalika, ofisa huyo alisema kuwa bado kuna tatizo kwa baadhi ya machinga ya kuvamia maeneo yasiyo rasmi ikiwamo kando kando ya barabara na kwenye mitaro ya kupitisha maji na kusababisha adha kwa watumiaji wengine.

Alisema halmashauri imetenga barabara zinazotumika kama soko la muda lakini si barabara zote.

Aidha, aliwataka wafanyabiashara hao kushirikiana na halmashauri ya jiji pale wanapogundua kuna baadhi yao wamekuwa wakikiuka maagizo ili wachukuliwe hatua.

“Pia kuna utapeli kwa baadhi ya wafanyabiashara wanaowalaghai wenzao kwa kuwauzia maeneo ambayo yapo wazi huku wakidai kuwa wana vibali halali toka halmashauri ya jiji jambo ambalo si la kweli,” alisema.

Chanzo: www.ippmedia.com


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.