• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Madaktari bingwa wa Benjamin Mkapa, kutoa huduma Iringa, wananchi changamkieni fursa

Imewekwa tarehe: February 15th, 2020

Timu ya madaktari bingwa wa hospitali ya Benjamin Mkapa kutoka Dodoma, inatarajiwa kutoa huduma za kibingwa za magonjwa ya njia ya mkojo, pua, koo na masikio ikiwemo watoto na mifupa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa kuanzia Jumatatu Februari 17.

Huu ni mwendelezo wa utoaji Huduma Tembezi  "outreach" inayofanywa na hospitali hiyo ikilenga kufikisha huduma za kibingwa kwa wananchi. Mwezi uliopita walikuwa Wilayani Kiteto mkoani Manyara ambako walitoa huduma za magonjwa ya moyo, upasuaji, njia ya mkojo na figo.

Kiongozi wa jopo la madaktari bingwa watakaotoa huduma mkoani Iringa Daktari Charles Lema, amesema kuwa watatoa huduma kwa siku 5. "Kwa hiyo tuwaombe wananchi wa Iringa na maeneo ya jirani, kuchangamkia hiyo fursa, kutakuwa na madaktari bingwa wa mifupa, madaktari bingwa wa magonjwa ya njia ya mkojo, madaktari bingwa wa magonjwa ya pua, koo na masikio, na madaktari bingwa wa watoto" amesisitiza Dkt. Lema.

Aidha, daktari huyo amesema kuwa watatumia fursa hiyo kutambulisha huduma zinazotolewa na Hospitali ya Benjamini Mkapa, ili kama kuna mtu anazihitaji asisite kufika na kupata huduma hizo. Huu ni mwendelezo wa mkakati wa Hospitali ya Benjamin Mkapa kuwafikia wananchi, tumetoka Kiteto na tutazidi kwenda maeneo mengine kadiri uhitaji utakavyokuwa unaonekana.

Akitoa ushuhuda wa huduma hizo, Hawa Rajabu mkazi wa Ngarenoro, amesema kuwa "Kwa wamama kama sisi tunashida za matumbo, lakini kama hivyo unaweza ukaenda mahali, wengine wanatumia hata mizizi. Lakini kutokana na madaktari waliokuja kwa utaalam wao tunavyowaeleza kwa kweli wanatusaidia tunashukuru kwa hilo. Tunaomba isiwe mara moja tu, waongeze ili wakati mwingine kwa mwaka iwe mara mbili au mara tatu ili wananchi waweze kusaidika zaidi."

Kwanza natoa shukurani kwa ujio wa madaktari hawa tunashukuru sana, maoni yangu nilikuwa napenda wawe wanatujia mara kwa mara kwa sababu hapa huduma zetu ni chache, huduma zinapatikana lakini nyingi si kama hivi ambazo tumezipata. Tunawashukuru sana hawa madaktari bingwa, watuijie mara kwa mara" amesema mkazi wa Kiteto Zubeda Hasan.

Jopo la madaktari bingwa wakiwa kazini wakati wakihudumia wananchi wa Kiteto.

Chanzo: maelezo tv online

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.