• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Madaktari wazawa BMH wapandikiza figo wenyewe, ni kwa mara ya kwanza nchini

Imewekwa tarehe: March 20th, 2020

HOSPITALI ya Benjamin Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma kwa mara nyingine imeandika historia, kwa madaktari wazawa peke yao kufaulu kupandikiza figo kwa ufanisi mkubwa. Madaktari hao wamefaulu kupandikiza figo kwa Emmanuel Kahigi, ambaye kwa miaka mitano hakuwahi kupata mkojo kutokana na figo yake kushindwa kufanya kazi.

Anakuwa mgonjwa wa 12 kupandikizwa figo BMH. Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma, Dkt. Alphoce Chandika akizungumza hospitalini hapo jana alisema upandikizaji huo umefanyika Machi 3, mwaka huu kwa ufanisi mkubwa na madaktari wazawa, ambao ni wa kwanza kufanywa na wazawa hospitali hapo na hapa nchini.

“Upandikizaji huo ni wa tano lakini wa kwanza kufanyika na madaktari wazawa wakati ule wa kwanza Machi 2018, wa pili Septemba 2018, wa tatu Agosti 2019 na wa nne Januari 2020 ulifanyika kwa ushirikiano baina ya madaktari bingwa wa Tanzania na taasisi mbili za Japan (Tokushukay Medical Corporation na Taasisi ya Wanawake wa Chuo Kikuu Japan),” alisema Dkt. Chandika.

Dkt. Chandika alisema upandikizaji wa figo kwa Kahigi wa Geita, ulifanyika kwa saa 10.30 ambapo utoaji figo kwa njia ya upasuaji ulifanyika kwa saa 5.30. Upandikizaji ulitumia saa 5.00 na ulikuwa na ufanisi mkubwa kutokana pia na umakini wa watalaamu wa dawa za usingizi.

“Upandikizaji huo unaofanyika kwa ushirikiano wa madaktari bingwa wa Hospitali ya Benjamin na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ulifanikiwa kutokana na mafunzo ya umahiri waliopata kutoka kwa madaktari wa Japan waliokuja nchini na  wale waliokwenda nchini huko,” alisema.

Alisema upandikizaji figo nchini, umepunguza gharama za wagonjwa kwenda India, ambako mgonjwa mmoja hupandikizwa kwa Sh milioni 100, gharama ambazo hospitalini hapo wanatibiwa wagonjwa wanne hadi watano. Daktari Bingwa wa Upasuaji, Dkt. Masumbuko Mwashambwa alisema walifanya upasuaji kwa saa 10.30 kutokana na madaktari wazawa kufanya kwa mara ya kwanza, hivyo walikuwa na tahadhari kubwa.

Dkt. Mashambwa ambaye ni Mhadhiri Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Dodoma, alisema pia walitumia muda mrefu kutokana na shida ya mtoaji figo kuwa na matatizo kwenye mshipa mmoja ambao ni muhimu katika kutoa figo. Pia alizitaka pia hospitali nyingine kama KCMC, Bugando na Mbeya kuiga BMH na kuanzisha huduma hizo za kupandikiza figo kutokana na matatizo hayo kuwa makubwa katika jamii.

Daktari wa Magonjwa ya Figo, Dkt. Kessy Shija alisema upasuaji huo kufanyika hospitalini hapo, umesaidia kupunguza gharama, ambazo angetumia kwenda kufanyiwa upandikizaji nje ya nchi. Dkt. Shija pia alipongeza timu ya wapandikizaji figo, ambao walionesha umahiri wa hali ya juu katika kuhakikisha mgonjwa anayepandikizwa figo, anakuwa salama pamoja na mtoaji.

Chanzo: Tovuti ya HabariLeo




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.