• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Magonjwa yasiyoambukiza hasara kubwa kwa taifa

Imewekwa tarehe: November 9th, 2020

Maisha ya watu yanafupishwa na magonjwa yasiyoambukiza kutokana na maradhi ya Moyo, Kisukari, Saratani, Magonjwa ya njia ya hewa, Siko Seli, ajali, magonjwa ya figo, akili, dawa za kulevya na magonjwa sugu ya meno na macho.

Hayo yamesemwa leo na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi (pichani) ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Afya wakati akifungua kongamano la pili la kitaifa la kisayansi la magonjwa yasiyoambukiza linalofanyika kwenye ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam.

Prof. Makubi amesema kuwa magonjwa hayo yamesababisha hasara kubwa kwa taifa kwa maana ya kuondoa nguvu kazi na kurudisha nyuma maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla na hivyo kusababisha utegemezi sugu kwa familia na pia kuongeza mzigo mkubwa kwenye mfumo wa afya kwa kuwa ni magonjwa ya muda mrefu na yanatumia rasilimali nyingi.

Akielezea hali ya magonjwa hayo Mganga Mkuu huyo alitaja takwimu za kitaifa zinaonesha kuwa magonjwa hayo yamesababisha asilimia 33 ya vifo vyote nchini kwa mwaka 2017, ambapo jumla ya vifo 134,600 viliripotiwa na kuhusishwa na magonjwa yasiyoambukiza.

“Vifo hivi vimetokana zaidi na magonjwa ya moyo na shinikizo la damu kwa asilimia 13, Kisukari 2%, Saratani 7% na ajali 11%, hali hii kwa ujumla haikubaliki na inatufanya tujumuike katika kujitathimini na kupanga mikakati ya pamoja ili kukabiliana na changamoto hii”. Alisisitiza Prof. Makubi.

Aidha, amesema takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO), magonjwa yasiyoambukiza yanachangia zaidi ya vifo milioni 41 ambayo ni sawa na asilimia 71 ya vifo vyote milioni 57 vilivyotokea mwaka 2016.

Aliongeza kuwa Magonjwa yasiyoambukiza yanachangia zaidi ya robo tatu (75%) ya vifo ambavyo kama ugonjwa ungetambulika mapema vingeweza kuepukika na huku mataifa ya uchumi wa kati na chini kama Tanzania yanaonekana kuathirika zaidi.

Hata hivyo Prof. Makubi aliwapongeza wanasayansi ambao wamewasilisha maandiko yao katika kongamano hilo ili kutoa ushahidi wa kisayansi wa ukubwa wa changamoto zilizopo katika kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza na ushauri wa namna ya kuzitatua.

Pichani chini ni baadhi ya washiriki wa kongamano la pili la kitaifa la kisayansi la magonjwa yasiyoambukiza linalofanyika kwenye ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam.


Chanzo: Wizara ya Afya

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.