• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mahenge awataka wananchi kuchangamkia fursa za uwekezaji Dodoma

Imewekwa tarehe: February 14th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge amewataka wawekezaji, wafanyabiashara na wananchi wa Jiji la Dodoma kuhakikisha wanachangamkia fursa za uwekezaji zilizopo katika Jiji hili linalokua kwa kasi ili kuweza kuendana na hadhi ya Makao Makuu yenye ubora katika sekta zote.

Kauli hiyo ameitoa katika kikao cha tathmini ya miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kilichofanyika katika ukumbi mdogo wa mikutano wa Halmashauri.

Dkt. Mahenge amesema wakati umefika sasa kwa wawekezaji kutambua na kuchangamkia nafasi zilizopo kwa kuitumia miradi hiyo, ambayo ina miundombinu rafiki ya kuwawezesha kufanikisha malengo yao katika utoaji huduma, pia kuwawezesha kuinua viwango vya huduma na kufanya viwe vya kimataifa ili kukidhi matakwa ya watumiaji.

“Dodoma kuna fursa nyingi, tuna miradi ya kimkakati ambayo iko katika hatua za mwishoni kumalizika ili ianze kutumika. Lipo soko, kituo cha mabasi, bustani ya mapumziko ya Chinangali, na kituo cha malori Nala, pia kuna miradi ambayo kulingana na Jiji letu kuwa Makao Makuu tumepata neema serikali itajenga uwanja wa ndege na kiwanja cha mpira vyote vyenye hadhi ya kimataifa.

“Lazima tuwe na mipango mikakati mizuri ya kuwawezesha wawekezaji wenye uthubutu wawekeze hapa, kwa sababu tuna miradi yenye viwango vya kimataifa hivyo ni lazima huduma zetu za afya, elimu, na huduma nyinginezo nazo tuziweke katika hadhi hiyo ili wageni mbalimbali wapate nafasi ya kufurahia uwepo wao ndani ya Jiji letu,” alisema Dkt. Mahenge.

Mbali na kuizungumzia miradi hiyo ya kimkakati Mkuu huyo wa Mkoa pia ametoa ushauri kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuhakikisha anaweka mipango thabiti itakayowezesha wananchi kufanya shughuli zao ikiwemo uuzaji na ununuzi wa bidhaa madukani, kuwa na miundombinu rafiki kwao na usalama wa mali zao.

“Utekelezaji wa hayo yote utatokana na mipango mizuri mtakayokuwa nayo, kwa mfano ukizunguka maeneo ya mjini kuanzia barabara 7 na kuendelea sehemu zote zilizotengwa kwa ajili ya maegesho ya wateja hivi sasa wamiliki wa maduka wamegeuza na kuweka magari yao wenyewe.

“Hali inayosababisha usumbufu kwa wateja wanapoenda na magari yao, lakini pia mnaweza kuongea na wahusika wa Shirika la Reli Tanzania ili wawapatie eneo la Jamatini mlitumie  kama eneo la maegesho  ambapo pia mtaingiza mapato, wateja wakilipa kwa masaa sio vibaya ili eneo la mjini libaki kuwa wazi bila msongamano wa magari” alisema Mkuu wa Mkoa huyo.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amemtaka Mkurugenzi kuweka usimamizi mzuri  ifikapo wakati wa zoezi la ugawaji wa maeneo katika miradi ya kimkakati kwa  wafanyabiashara watakaopatiwa nafasi, na zoezi liendeshwe kwa umakini, uhuru na haki ili kuepukana na madalali watakaoweza kujitokeza na kulitia doa zoezi hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge alipotembelea Jiji la Dodoma akiambatana na Katibu Tawala wa Mkoa, na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Patrobas Katambi na maafisa kutoka ofisi yake. Pichani anaonekana Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi (aliyesimama) akimukaribisha ujumbe huo.

 

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Patrobas Katambi (katikati) akipokea makablasha yenye maelezo kuhusu miradi ya uwekezaji na uendeshaji wake kutoka kwa Mkurugenzi wa Jiji Godwin Kunambi.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.