• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Majaliwa aagiza mikakati endelevu ya Mazingira Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: June 2nd, 2021

IKIWA ni Wiki ya Mazingira, Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa ameuagiza uongozi wa Jiji la Dodoma kuhakikisha wanaweka mikakati endelevu ya uhifadhi mazingira kwa kuhakikisha maeneo yote yanayopimwa yanapandwa miti.

Hatua hiyo imekuja kufuatia ripoti ya Mazingira nchini kuonyesha kiwango cha ukataji miti katika mkoa huo kuwa ni wastani wa hekta 3,730,000 kwa Mwaka kiasi ambacho amekitaja kuwa ni kikubwa sana kinachopelekea hali ya ukame zaidi.

Hayo yameelezwa jana Jijini hapa na Waziri Mkuu wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya mazingira duniani ambalo hufanyika kuanzia Juni 1 hadi 5, 2021 kwa lengo la kuikumbusha jamii umuhimu wa uhifadhi mazingira.

 Akiongea kwenye uzinduzi huo amesema kutokana na  ripoti ya mazingira kuonyesha kuwa Dodoma ni mkoa unaokabiliwa na ukame nchini, uongozi huo uhakikishe kila mwananchi anayepata kiwanja anaelimishwa kuhusu umuhimu wa kupanda miti ili kuunusuru mkoa wa Dodoma na hali ya ukame.

 Amesema changamoto nyingi za mazingira zimeonekana katika Mkoa wa Dodoma hivyo kuutaja mkoa huo kuwa mwenyeji wa Maadhimisho hayo Kitaifa yanayoyarajiwa kuwafanyika Juni 5.

"Kutokana na ripoti ya mazingira kuonyesha kuwa Dodoma ni kame kwa mwaka huu Serikali imeamua kufanya Maadhimisho Kitaifa Mkoani hapa ili kuwakumbusha wakazi wake kuwa makini kwa utunzaji mazingira," alisema.

Kutokana na hayo Waziri Majaliwa alitolea mfano wa ripoti ya tatu ya hali ya mazingira nchini iliyofanyika mwaka 2019, ikionyesha Dodoma Kuwa ni miongoni mwa maeneo ya ukame na yana kasi kubwa ya ukataji wa miti.

"Ni wakati sasa wa kuendelea kubuni nishati mbadala, kiwango hicho kinaonyesha kusababishwa na mahitaji makubwa ya nishati ya kuni na mkaa, lazima tushirikiane kuhakikisha Dodoma inakuwa ya kijani,"alisisitiza.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Selemani Jafo ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa katika Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira, shughuli mbalimbali zitafanyika ikiwemo maonesho ya mazingira kupitia taasisi zaidi ya 100.

"Katika maonyesho hayo wakazi wa Dodoma watapata nafasi ya kujifunza teknolojia mbalimbali za nishati mbadala ili kuondokana na uharibufu wa mazingira kwa kukata miti kwa matumizi ya nyumbani," alisema Jafo.

Pamoja na hayo aliongeza kuwa wiki hiyo pia itahusisha semina itakayowashirikisha maofisa mazingira nchini kutoka katika wizara, taasisi na mamlaka za Serikali za mitaa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.