• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Majaliwa apiga marufuku vyakula vya nje migodini

Imewekwa tarehe: January 27th, 2020

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha kuanzia sasa vyakula kwenye migodi havitoki nje ya nchi na badala yake watumie vinavyozalishwa nchini.

Pia amekemea ukamataji holela wa wawekezaji na wadau wa madini, akivitaka vyombo vya ulinzi na usalama kufuata sheria, kanuni na miongozo inayosimamia sekta hiyo.

Majaliwa alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akifunga semina maalum ya vyombo vya ulinzi na usalama kuhusu usimamizi wa rasirimali madini iliyofanyika jijini hapa.

Alisema katika kipindi cha hivi karibuni, kumejitokeza malalamiko mengi kutoka kwa wawekezaji na wadau wa madini kuhusu kukamatwa au kubughudhiwa bila sababu za msingi.

"Natumia nafasi hii kukemea suala la ukamataji holela wa wawekezaji au wadau wa madini pasipo kufuata taratibu. Hivyo basi, tumieni sheria, kanuni na miongozo mbalimbali iliyowekwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha usimamizi wa sekta ya madini," aliagiza.

Alisema uanzishaji wa masoko ya madini ni sehemu ya mkakati mahsusi wa serikali kupunguza utoroshwaji wa madini kwa kuwa awali ilionekana kuna utoroshaji mkubwa unaofanyika kwa kisingizio cha kutafuta soko.

"Hata hivyo, kuna tatizo lingine limeanza kujitokeza la kuwakamata wadau wakiwa na madini hata kama wanapeleka sokoni," alisema.

Aliagiza kuanzia sasa wadau wote wanaopatikana na madini, wapewe utaratibu wa kuelekea sokoni kuuza badala ya kuwakamata wakiwa wanaenda sokoni.

"Ni wajibu wetu kusimamia na kudhibiti utoroshwaji wa madini na pia ni jukumu letu sisi kama vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha kuwa masoko haya pamoja na wafanyabiashara ya madini wanaofanya kazi zao kwa kufuata sheria wanalindwa na kuepuka kamata kamata zisizo na tija," aliagiza.

Alisema kuna wakati hawahitaji kutumia nguvu nyingi bali kutoa ushauri tu ili kutatua shida husika.

Kuhusu vyakula, Waziri Mkuu alisema vyombo hivyo vinapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha huduma za vyakula migodini kuanzia sasa hazitoki nje ili bidhaa zilizopo nchini zitumike.

"Unakuta mchele wanaoutumia wafanyakazi wa migodini unatoka nje, jambo ambalo halikubaliki kwa sababu mchele tunalima sisi wenyewe, hivyo naagiza suala hilo likafanyiwe mabadiliko," alisema.

Waziri wa Madini, Dotto Biteko, alitangazia 'vita' dhidi ya watu wanaouza madini feki na kuwataka waache mara moja kwa kuwa tayari wamewabaini.

"Tunaomba wanaofanya hivyo waache mara moja, tunaanza msako wa kuwatafuta watu wa aina hii," alionya.

Chanzo: www.ippmedia.com


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.