• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Majaliwa: Serikali itaendelea kujenga uhusiano mzuri wa kijinsia

Imewekwa tarehe: November 10th, 2021

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan itaendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuhakikisha inajenga uwiano mzuri wa kijinsia na wanawake katika uongozi na ngazi nyingine za maamuzi.

“Nitumie fursa hii pia kutambua mchango mkubwa wa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kujenga uwiano wa kijinsia na wanawake katika uongozi”.

Amesema hayo leo (Jumatano, Novemba 10, 2021) alipomuwakilisha Rais Samia katika ufungaji wa Jukwaa la Uongozi wa Vijana kwa mwaka 2021 lilifanyika katika Chuo cha Maendeleo na Ushirikiano wa Kimataifa (MS TCDC) jijini Arusha.

Amesema katika teuzi alizozifanya hivi karibuni, Mheshimiwa Rais Samia aliteua majaji wanawake 13 kati ya 28 wa Mahakama Kuu sawa na asilimia 43 na hivyo, kufanya idadi ya majaji wote nchini kufikia wanawake 40 kati ya majaji wote 86. “Ukiachilia mbali Katibu wa Bunge mwanamke, Mheshimiwa Rais pia aliteua Makatibu Tawala wa Mikoa wanawake 12 kati ya 26 sawa na asilimia 46”.

Mheshimiwa Majaliwa amesema  Tanzania imeendelea kupiga hatua kubwa katika kuhakikisha inajenga uwiano mzuri wa kijinsia na wanawake katika uongozi na ngazi za maamuzi. “Kwa mfano katika uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani wa mwaka 2015, tulikuwa na wabunge wanawake 127 ikilinganishwa na wabunge wanawake 143 mwaka 2020”

Waziri Mkuu amesema kuwa ili kukabiliana na changamoto ya ajira Tanzania iliamua kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025 ambayo pamoja na mambo mengine inalenga kujenga uchumi wa kati wa viwanda na hivyo, kutengeneza ajira kwa kufungamanisha sekta hiyo na sekta nyingine za uchumi ikiwemo kilimo, madini, maliasili na utalii na sekta ya ujenzi.

Ameongeza kuwa juhudi hizo zimeonesha mafanikio baada ya Julai 2020 Tanzania kuingia kwenye kundi la nchi zenye uchumi wa kati wa chini. “Mafanikio hayo, yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na sera nzuri na fedha na uchumi jumla sambamba na matumizi sahihi ya rasilimali tulizo nazo na kuwa kwenye eneo la kimkakati kijiografia.”

Aidha, Waziri Mkuu ametoa wito kwa kwa wakuu wa nchi na Serikali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Umoja wa Afrika na sekta binafsi kuongeza juhudi katika kujenga usawa wa kijinsia na wanawake katika uongozi na ngazi nyingine za maamuzi.

Pia Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua mchango wa vijana katika kukuza uchumi hivyo ni muhimu vijana wakaendelea kujituma, kujitoa, na wawe waadilifu ili kujenga Taifa adilifu hasa wanaposhiriki katika matukio mbalimbali ya uzalishaji mali.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Peter Mathuki amesema atahakikisha anayafikisha mawazo yote yaliyotolewa na vijana hao kwa watunga sera katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ili yaweze kufanyiwa kazi kwa maendeleo ya vijana na jumuiya kwa ujumla.

Kadhalika, kiongozi huyo amewaomba viongozi mbalimbali waendelee kuwafundisha na kushirikiana na vijana hao ili waweze kujifunza zaidi na kuwa viongozi bora hapo baadaye.

Chanzo: Ofisi ya Waziri Mkuu

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.