• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Makamu wa Rais azindua Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021

Imewekwa tarehe: February 12th, 2022

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango leo tarehe 12 Februari, 2022 amezindua Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, uzinduzi uliofanyika katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.

Makamu wa Rais amesema kazi ya kuhifadhi mazingira ikiwemo kulinda vyanzo vya maji, misitu, upandaji miti, kupendezesha miji, kufanya kusafi katika maeneo yote ya makazi na biashara, viwandani na masokoni ni lazima kuanzia sasa kuwa kazi za kudumu. Aidha amesema viongozi wote kuanzia ngazi ya vijiji hadi mikoa wanapaswa kusimamia uhifadhi wa mazingira na suala hilo litakua kipimo cha utekelezaji wa majukumu yao.

Aidha, Makamu wa Rais amesema ni muhimu kuondoa nadharia katika uhifadhi wa mazingira ikiwemo kuwa na mipango isiyotekelezwa bali inahitajika kazi ya ziada itakayotoa matokeo chanya katika kuhifadhi mazingira. Amesema sheria ndogondogo za uhifadhi wa mazingira zinapaswa kusimamiwa ikiwemo faini na ikiwezekana kuongeza faini hizo ili kukomesha waharibifu wa mazingira. Dkt. Mpango amesema zoezi la kutunza mazingira lazima kuwa shirikishi kwa wadau wote kuanzia mijini na vijijini na kuagiza wizara na taasisi zote za serikali kuhakikisha wanapanda miti na kuitunza katika maeneo yao.

Makamu wa Rais amewataka Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) kutoa elimu kwa wananchi juu ya aina ya miti inayopaswa kupandwa kulingana na maeneo wanayoishi. Aidha amewaasa kuhakikisha wanaongeza miche itakayopandwa ikiwemo kuongeza vitalu katika maeneo mbalimbali ili wananchi wapate urahisi wa kupata miche hiyo.

Vile vile, Makamu wa Rais ametoa wito kwa wamiliki wa viwanda nchini kuzingatia misingi ya uzalishaji endelevu pamoja na kutumia teknolojia rafiki kwa mazingira ili kupambana na uchafuzi wa mazingira.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais ameagiza Wizara ya Ardhi, Wizara ya Maji, Wizara ya Kilimo , Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha wanashirikiana kushughulikia suala la uharibifu wa mazingira unaofanywa kwenye chanzo cha mto Ruaha katika Bonde la Ihefu kutokana na kuingizwa kwa makundi makubwa ya mifugo pamoja na kuelekezwa maji katika mashamba makubwa bila kurejeshwa mtoni.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Dkt. Selemani Jafo amesema Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021 imezingatia masuala mbalimbali ikiwemo mpango wa taifa wa miaka mitano, mpango endelevu, pamoja na mpango wa miaka 15 ulioanza 2011-2012. Amesema sera hiyo inatarajiwa kuokoa uharibifu wa mazingira katika nchi pamoja na kuongeza fursa za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa jumla.

Amesema tayari wizara imefanya zoezi la utoaji elimu ya uhifadhi wa mazingira na kuongeza kwamba kwa muda wa siku tano tayari jumla ya miti laki moja na elfu arobaini na moja imepandwa katika jiji la Dodoma pekee huku lengo likiwa ni kupanda miti milioni 14.5 nchi nzima kwa kuwashirikisha wanafunzi nchi nzima.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Marry Maganga amesema maandalizi ya Sera ya Taifa ya Mazingira ya Mwaka 2021 yametokana na kuongezeka kwa changamoto mpya za uharibifu wa mazingira ikiwemo uchafuzi wa mazingira unaotokana na taka zitokanazo na vifaa vya umeme, matumizi ya kemikali yasioendelevu, mabadiliko ya tabia ya nchi pamoja na changamoto ya shughuli za uchimbaji wa mafuta , madini na gesi.

Naye Mwenyekiti kamati ya kudumu ya Bunge ya Uwekezaji, Viwanda, Biashara na Mazingira David Mwakiposa Kihanzile amesema ni muhimu serikali kuanza haraka mchakato wa kutungia sheria na kanuni sera hiyo ili ianze kutekelezwa kwa ufanisi. Amesema suala la upandaji miti linapaswa kuwa na mkakati maalum utakaorahisisha zoezi hilo.





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.