• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Makao Makuu Dodoma kujengwa na watu wote

Imewekwa tarehe: December 4th, 2021

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inaamini kuwa makao makuu ya nchi yanajengwa na watanzania wote na wawekezaji mbalimbali kwa lengo la kutanua wigo wa ajira na kusogeza huduma kwa wananchi.

Kauli hiyo ilitolewa na kiongozi wa timu ya kimkakati ya Uwekezaji na Masoko ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Leonard Machunde (pichani) katika ukumbi wa Shirikisho la wenye Viwanda Tanzania (CTI) jijini Dar es Salaam.

Machunde alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ndiyo Makao Makuu ya nchi. “Makao makuu ya nchi, hayajengwi tu na wakazi wa Dodoma”. Makao Makuu yanajengwa na watanzania wote na wawekezaji mbalimbali wa ndani na nje ya nchi. Ndiyo sababu halmashauri iliunda timu hii ili ifikishe ujumbe huo kwa Watanzania wote” alisema Machunde.

Akiongelea fursa za uwekezaji zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Machunde alisema kuwa halmashauri hiyo imetenga eneo la ujenzi wa viwanda Nala. Alisema kuwa eneo hilo lina viwanja vyenye ukumbwa wa kuanzia hekari moja hadi 100. Ujenzi wa viwanda ni fursa muhimu katika kuzalisha ajira,biashara na unachochea usogezaji wa huduma kwa wananchi, aliongeza.

Machunde ambae pia ni mbobezi katika tasnia ya Fedha na Uwekezaji alisema kuwa uwekezaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni kitendo sahihi. “Bahati nzuri ukinunua kiwanja katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma unakuwa umenunua kiwanja serikalini. Fedha inayolipwa, inalipwa Serikalini kupitia namba ya udhibiti (control number) na hakuna mtu wa kati wa kupandisha gharama. Hivyo, unakuwa katika mikono salama ya serikali” alisema Machunde kwa kujiamini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Maendeleo ya Wanachama na Huduma wa Shirikisho la wenye viwanda Tanzania, Neema Mhondo aliipongeza timu hiyo kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kazi nzuri. Alisema kuwa wawekezaji wanapenda sana kufahamu kama eneo lililotengwa kwa ajili ya uwekezaji lina miundombinu muhimu ya kuwezesha viwanda kujengwa. Miundombinu hiyo ni umeme, maji na barabara. Alisema kuwa miundombinu hiyo ni muhimu kwa sababu inapunguza gharama za uendeshaji.

Nae Afisa Mipango Miji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Aisha Masanja alisema kuwa eneo la viwanda Nala lina miundombinu wezeshi na ya uhakika kwa ajili ya ujenzi wa viwanda. Maji na umeme wa msongo mkubwa upo kwa ajili ya viwanda. “Eneo hilo la viwanda Nala lipo kilometa tatu kutoka barabara kuu ya kutoka Dodoma kuelekea Singida na likiwa umbali wa kilometa moja na nusu kutoka barabara ya mzunguko wa nje” alisema Masanja.

Kiongozi wa timu ya kimkakati ya Uwekezaji na Masoko ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Leonard Machunde akifafanua jambo

 

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Wanachama na Huduma wa Shirikisho la wenye viwanda Tanzania, Neema Mhondo (kulia) akiongea na timu ya kimkakati ya Uwekezaji na Masoko ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ukumbi wa mikutano wa CTI jijini Dar es Salaam.

Timu ya kimkakati ya Uwekezaji na Masoko ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ikiongozwa na Leonard Machunde Mpima Ardhi (wapili kushoto). Wa kwanza kushoto ni Ahmed Msangi Mchumi Mwandamizi, Aidha Masanja, Afisa Mipango Miji (wa pili kulia) na Mary Ngowi, Afisa Ardhi (wa kwanza kulia) walipotembelea Shirikisho la wenye viwanda Tanzania (CTI) kuelezea fursa za uwekezaji katika viwanda zilizopo jijini Dodoma

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.