• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Makatibu Mahsusi Jiji warejea, waahidi 'kazi inaendelea'

Imewekwa tarehe: May 24th, 2021

MAKATIBU MAHSUSI nchini wametakiwa kuwa na lugha ya staha wakati wa kutoa huduma kwa umma wakati wa mkutano wao wa mwaka ambapo na Makatibu Mahsusi 3000 wameshiriki Mkutano huo wakiwemo 11 kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mkutano huo ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo ulifunguliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye aliwakumbusha Makatibu Mahsusi nchini kutumia lugha yenye staha wakati wa kuwahudumia watumishi na wananchi wanaofuata huduma katika taasisi zao.

Wakihojiwa na Tovuti hii ya Jiji kwa nyakati tofauti, Makatibu Muhtasi hao wa Halmashari ya Jiji la Dodoma kila mmoja alikumbusha yale waliyoyapata kwenye mkutano huo ambayo yameamsha ari kubwa kwao kufanya kazi kwa bidii na kusisitiza kauli mbiu ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kuwa ‘Kazi Iendelee’.

Kwa upande wake Joyce Kiula alisema kuwa, “Mhe. Mchengerwa alitukumbusha Makatibu Mahsusi kuwa sisi ni kioo cha ofisi yetu ambapo wageni wanaofuata huduma wanapata taswira halisi ya huduma zinazotolewa na taasisi yetu, hivyo tunapaswa kuwa na kauli nzuri na kutoa huduma bora kwa wageni na wananchi”.

Naye Scola Njawa, ambaye ni Katibu Muhtasi wa Ofisi ya Mweka Hazina wa Jiji la Dodoma, alisema kuwa Mhe. Mchengerwa aliwaambia kuwa hakuna haki isiyokuwa na wajibu. “Kwa msingi huo Waziri ametutaka Makatibu Mahsusi kutofanya kazi kwa mazoea na wale ambao ni kikwazo katika kutoa huduma wabadilike ili kuendana na azma ya Serikali.”

“Mimi kwa upande wangu nilishika sana maneno ya Mhe. Mchengerwa alivyotuasa Makatibu Mahsusi kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia uadilifu hususan utunzaji wa siri za ofisi na akatuonya kuwa watakaobainika kutozingatia taratibu za kazi zetu basi wataondolewa katika ofisi zao” alisema Wankaela Timotheo kutoka ofisi ya Afisa Elimu Sekondari wa Jiji la Dodoma.

Aidha, Maula Komba wa Idara ya Ujenzi alisema kuwa amefurahishwa na kauli ya Mheshimiwa Mchengerwa aliposema kuwa Serikali inatambua umuhimu wa Makatibu Mahsusi katika uendeshaji wa shughuli za kila siku za ofisi, hivyo hawana budi kuendelea kuilinda imani ya Serikali kwa kuwajibika kikamilifu.

Edina Charles wa Ofisi ya Afisa Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika akimkunukuu Mhe. Mchengerwa alisema “Tunahitaji watumishi wachapakazi na waadilifu, kwani dhamira ya serikali ni kusonga mbele, kama utashindwa kufanya kazi kwa bidii na uadilifu utaondolewa bila kujali taasisi uliyopo.” Alisema Edina akionesha kujali sana kauli ya Mhe. Mchengerwa.

Kwa upande wake Fatina Sharifu Katibu Mahsusi wa Mradi wa Uboreshaji Miji wa Kimkakati (TSCP) alisema “Mimi nakumbuka Mhe. Waziri Mchengerwa alihimiza kuhusu uadilifu na alitutaka Makatibu Mahsusi kula kiapo cha Uadilifu kwa Watumishi wa Umma ambapo wote tulitekeleza.

Katika hotuba ya ufunguzi kuna mengi yalisemwa, alianza kuongea Lucy Msigwa Katibu Mahsusi wa Kitengo cha Sheria mojawapo ni suala la waajiri kuthamini umuhimu wa Makatibu Mahsusi wenye umri mkubwa ambao wamekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya ofisi kwa kutumia uzoefu walio nao ikiwa ni pamoja na uadilifu na uchapakazi wao.

Neema Baseke Katibu Mahsusi ya Idara ya Mipango miji, Ardhi na Maliasiri alisema kuwa “Ili kuendana na Kaulimbiu ya mwaka huu inayohimiza ubunifu, umahiri na uzingatiaji wa weledi katika utendaji kazi kwa Makatibu Mahsusi, tunatakiwa kuitekeleza kwa vitendo kwa kujiendeleza kitaaluma” na Katibu Mahsusi Asia Bwesa alisisitiza kuwa wamejipanga kuyafanyika kazi yale yote waliyoambiwa na kwamba yamewakumbusha wajibu wao na kuamsha ari ya utendaji kazi, "tutajisikia furaha sana kuwa mfano bora kwa wenzetu na kutoa huduma bora kwa wananchi kwa faida ya taasisi yetu na wanaDodoma na wanachi wote kwa ujumla" alimalizia Asia.

Shamimu Makongoro wa Idara ya Utawala alirejea maneno ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. John Mongella kuhusu umuhimu wa Makatibu Mahsusi kiutendaji kiasi kwamba wakiondolewa hata kwa siku moja, utekelezaji wa majukumu ya taasisi yoyote ile utayumba.

Akiongea na tovuti hii Fatuma Kuchele wa Idara ya Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji amesema kada ya Uhazili tunatambua muhimu wetu kwa viongozi na watumishi wengine katika utendaji kazi wa kila siku, na Asia Bwesa akamalizi kuwa “hivyo tunatakiwa kuendelea kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ikiwa ni pamoja na kutunza siri za ofisi ili kusukuma gurudumu la maendeleo mbele”.

Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA) kilianzishwa mwaka 2008 kwa lengo la kukuza na kudumisha taaluma ya Makatibu Mahsusi na kuhimiza uwajibikaji ili kutoa huduma bora kwa umma na mkutano wa mwaka huu wa TAPSEA uliongozwa na kauli mbiu isemayo “Kuwa Mbunifu Mahiri, Zingatia Weledi katika Kuleta Mabadiliko ya Uchumi Tanzania.”


Makatibu Mahsusi wa Jiji la Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja waliporejea kwenye kituo chao cha kazi baada ya kuhudhuria mkutano wao mwaka, kutoka kushoto ni Fatuma Kuchele, Joyce Kiula, Scola Njawa, Edina Charles, Asia Bwesa, Neema Baseke na Wankaela Timotheo. 

Makatibu Mahsusi wa Jiji la Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja kutoka kushoto ni Lucy Msigwa, Fatina Sharifu, Maula Komba, Shamimu Makongoro, Fatuma Kuchele, Joyce Kiula, Scola Njawa na Edina Charles.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.