• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Makatibu Wakuu wakoshwa na maendeleo ya ujenzi wa mradi wa reli Dodoma - Morogoro

Imewekwa tarehe: March 3rd, 2020

Makatibu Wakuu na Naibu Makaribu wa wizara tofauti nchini pamoja na sektetarieti ya baraza la mawaziri wakiongozwa na mwakilishi wa Katibu Mkuu kiongozi Mhe. Prof. Sifuni Mchome wametembelea mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa - SGR kipande cha Dodoma - Morogoro jana tarehe 2 Machi 2020.

Lengo la ziara hiyo ya siku mbili  yaani tarehe 2-3 ni kuona maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa – SGR kuanzia Dodoma hadi Dar es Salaam kwa kipande cha Morogoro - Dodoma - Singida  chenye urefu wa Kilometa 422 ambao umefikia zaidi ya 28% na Dar es Salaam – Morogoro umbali wa Kilometa 205 ambao umefikia zaidi ya 75%.

Ziara hiyo ilianza Mkoani Dodoma ambapo Makatibu wakiwa na mwenyeji wao Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania - TRC Ndugu Masanja Kungu Kadogosa walitembelea katika maeneo mbalimbali ya mradi ikiwemo kambi kubwa ya mradi wa SGR iliyopo Ihumwa Dodoma, mahahandaki 4 yanayojengwa Kilosa mkoani Morogoro, kiwanda cha uzalishaji wa mataruma chenye uwezo wa kuzalisha mataruma 1100 kwa siku kilichopo eneo la Kilosa pamoja na kuona kazi za ujenzi wa tuta, madaraja, makalavati na uwekaji mataruma, reli na nguzo za umeme kwenye tuta la reli

Akiongea katika ziara hiyo Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano sekta ya uchukuzi Dkt. Leonard Chamuriho amesema kuwa Mkandarasi anapiga hatua katika ujenzi na usanifu wa njia ya Reli na kazi kubwa inafanyika usiku na mchana.

“Ziara yetu hii ni ya siku mbili Machi 2 - 3, 2020, leo tumetembelea kipande cha Makutupora hadi Morogoro tumeona kazi kubwa inafanyika kwa kasi katika ujenzi wa mahandaki manne, kesho tutatembelea kipande cha Dar es Salaam – Morogoro, kazi inakwenda vizuri na tunatarajia itakwisha kwa wakati” alisema Chamuriho

Naye mwenyeji wa msafara Mkurugenzi Mkuu wa TRC Masanja Kadogosa amesema kuwa “Sisi kama TRC tunashukuru, ujio huu wa makatibu wa serikali katika mradi huu ambao ni mtambuka ambao unagusa wizara zote, kwahiyo ni ugeni muhimu sana kwa sababu utarahisisha utekelezaji wa mradi huu kwa kuwa watendaji wa wizara tayari watakuwa na uelewa juu ya changamoto na fursa zilizopo katika mradi, hawa ni watu ambao tunafanya nao kazi moja kwa moja”

Aidha Kadogosa amewahakikishia watanzania kuwa mradi wa SGR unaendelea vizuri na utakamilika, “Nawahakikishia watanzania kuwa mradi huu kipande cha Dar es Salaam – Morogoro tumebakisha 25%, hivyo mwaka huu treni lazima itapita na watanzania watapanda kwa mara ya kwanza, tunaendelea vizuri na tuna uhakika 100%” aliongeza Kadogosa.

Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara Prof. Riziki Shemdoe amesema kuwa  kitu ambacho amekiona katika mradi wa SGR angetamani kila mtanzania aje aone, kwa kuwa kazi iliyofanyika ni kubwa sana, amemshukuru Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa maamuzi magumu aliyochukua. Ujenzi huu umewanufaisha sana wawekezaji wadogo wadogo, wakulima na wafugaji wakati wa ujenzi na pindi utakapokamilika.

Makatibu hao wameonesha kufurahishwa na maendeleo ya mradi huo na namna ambavyo umesanifiwa kwa kuzingatia mazingira ya kitanzania pamoja na namna ambavyo wananchi wameshirikishwa moja kwa moja katika usanifu na ujenzi wa miundombinu ya reli hiyo ikiwemo vivuko vya magari, wanyama na watembea kwa miguu. Mradi huu utakapokamilika unatarajiwa kuleta manufaa kwa Shirika na uchumi wa taifa kwa ujumla kupitia usafiri wa abiria na usafirishaji wa mizigo.

Tazama picha mbalimbali wakati wa ziara hiyo:











Chanzo: Habari na picha kwa msaasa wa Idara ya Habari Maelezo

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.