• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mama Samia ajiandikisha Jijini Dodoma, awaomba wananchi kujitokeza.

Imewekwa tarehe: October 9th, 2019

WANANCHI wametakiwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika vituo vya uandikishaji na siku ya kupiga kura ili kuchagua viongozi wanaoendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Kauli hiyo ya hamasa imetolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan muda mfupi baada ya kujiandikisha katika kituo cha Shule ya msingi Dodoma Mlimani, iliyopo katika Mtaa Salimin, Kata ya Tambukareli jijini Dodoma leo asubuhi.

Mama Samia amewaomba wananchi wote kujitokeza na kujiandikisha katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019. Amewataka pia kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura ili kuchagua viongozi watakaowasimamia katika mitaa yao. “Mimi nimekuja kujiandikisha kwa sababu makazi yangu ni hapa Dodoma, na hawa ndio watanisimamia mambo yangu” amesema Mama Samia. Aidha, amewataka wananchi kuchagua viongozi wenye maadili mema na watakaowatumikia watanzania na kutunza rasilimali za nchi. Sifa nyingine za viongozi watakaochanguliwa alizitaja kuwa ni dhamira ya kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi na kwenda na kasi ya Serikali ya awamu ya tano.  

Awali akimkaribisha Makamu wa Rais, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge alisema kuwa Mkoa wa Dodoma unatarajia kuandikisha wananchi 900,000, ukiwa na vituo 3,679. Alisema kuwa siku ya kwanza ya uandikishaji tarehe 8 Oktoba, 2019 jumla ya wananchi 156,000 waliandikishwa.  

Uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2019 utafanyika tarehe 14 Novemba, 2019 ukiongozwa na kaulimbiu isemayo “Viongozi bora wa Serikali za Mitaa ni chachu ya maendeleo, ni haki na wajibu wako kujiandikisha, kugombea na kuchagua kiongozi kiongozi bora”.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suhulu Hassan (katikati) akizungumza na waandishi wa habari mara tu baada ya kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga kura Jijini Dodoma leo. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Binilith Mahenge na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Uchaguzi wa Jiji la Dodoma Hidaya Maeda.


Makamu wa Rais Mhe. Samia Suhulu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Mwandikishaji wapiga kura wa Mtaa wa Salimini, Kituo cha Shule ya Msingi Dodoma Mlimani bi. Asha Bakina Mussa leo Jijini Dodoma kabla Mama Samia hajajiandikisha kwenye Daftari la Wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.