• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Manispaa ya Iringa yajipanga kuwekeza jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: December 7th, 2020

HALMASHAURI ya Manispaa ya Iringa inajipanga kuanza kufanya uwekezaji mkubwa katika Jiji la Dodoma kwa lengo la kuongeza mapato yake na kukuza utoaji wa huduma kwa wananchi wake.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Hamid Njovu alipokuwa akiongea na timu ya wataalam wa kutangaza fursa za uwekezaji kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma walipomtembelea ofisini kwake kuishawishi manispaa yake kuwekeza Dodoma.

Njovu aliishukuru Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kupanga ziara ya kuhamasisha wawekezaji wa Manispaa ya Iringa kuwekeza jijini Dodoma. “Kwetu kama Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na kwangu kama Mkurugenzi wa Manispaa nimeona ni jambo zuri na nimeomba andiko pamoja na wasilisho lenu ambavyo nitaviwasilisha kwenye timu yangu ya wataalam kwa lengo la kuhakikisha wataalam wetu wanafikiria tofauti, kwamba sisi tunaweza kuwekeza katika Jiji la Dodoma” alisema Njovu.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa ni wakati muafaka kwa Manispaa ya Iringa ikajenga hoteli katika Jiji la Dodoma. “Ni vizuri sana tukawa na hoteli katika Jiji la Dodoma ili tunapotengeneza mnyororo wa watalii wetu watoke Dodoma waje Iringa, kwenda katika Hifadhi ya taifa ya Ruaha na maeneo mengine ya vivutio iwe rahisi zaidi. Kwangu mimi, nazishauri sana Halmashauri, kuna Halmashauri za Wilaya au Halmashauri za Miji zina mapato makubwa sana, lakini uwezo wao wa mapato upo katika mazao ya kudumu au mazao ya biashara. Ni muda sahihi wa kufikiria kubadilisha uwekezaji na kuhama na kuwekeza Dodoma, tusitegemee haya mazao na ushuru tuliouzoea wa masoko, ipo siku tunaweza kuachana na ushuru huo” alisema Mkurugenzi Njovu.

Awali akielezea fursa za uwekezaji zilizopo jijini Dodoma, Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Zainab Manyike alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imepima viwanja katika maeneo ya kimkakati kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Viwanja hivyo vipo kwa ajili ya ujenzi wa hoteli vinavyopatikana katika maeneo ya Mtumba, Iyumbu, Njedengwa na Kitelela, aliongeza. “Vipo viwanja kwa ajili ya ujenzi wa taasisi mbalimbali za serikali na binafsi katika eneo la Mtumba, Nala, Kikombo, Iyumbu, Nzuguni, Chahwa na Kitelela. Mkurugenzi nikwambie tu, hata Halmashauri ya Jiji la Dodoma inajenga hoteli yake ya ghorofa 11 kwa mapato ya ndani ikiwa katika hatua za mwisho kukamilika. Hivyo, Manispaa yako pia inaweza kwenda kujenga hoteli katika Jiji la Dodoma na kuongeza mapato yake. Na bahati nzuri, viwanja hivi vipo Halmashauri na hakuna dalali” alisisitiza Manyike kwa kujiamini.  

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeamua kutoka ofisini na kuwafuata wawekezaji katika maeneo yao kuelezea fursa zilizopo kwa lengo la kuwavutia kuwekeza jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Hamid Njovu (kushoto) akielezea mpango wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kuwekeza Jijini Dodoma mbele ya timu ya wataalam wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Afisa Ardhi Nuru Maliki (kulia) na Afisa Maendeleo ya Jamii Zainabu Manyike (katikati) ofisini kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.