• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Marufuku hospitali kuzuia maiti - Waziri Ummy

Imewekwa tarehe: February 14th, 2020

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, amepiga marufuku hospitali nchini kuzuia maiti kutokana na gharama za matibabu na badala yake zibuni njia mbadala za kudai malipo hayo.

Katazo hilo alilitoa jana jijini Dar es Salaam, alipofanya ziara katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Tawi la Mloganzila, kuangalia kero na vikwazo wanavyopata wagonjwa wanaopatiwa matibabu.

Alisema anafahamu lipo tatizo la wananchi kushindwa kumudu gharama za matibabu na ikizingatiwa kuwa hospitali hiyo inatoa huduma kwanza kabla ya kudai malipo.

"Ni marufuku hospitali kuzuia maiti kwa sababu mgonjwa alishindwa kulipa deni. Watafute utaratibu mwingine wa deni kulipwa bila kuzuia maiti," aliagiza.

Ummy alitoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wagojwa wanaodaiwa hospitalini hapo baada ya kupatiwa matibabu na hali zao kuimarika.

Alisema hilo ni tatizo katika hospitali nyingi nchini na kwamba serikali inafanyia kazi kuhusu namna ya kuwezesha wananchi wote kupata huduma za matibabu.

Waziri huyo alisema wameshatoa mapendekezo serikalini kuhusu bima ya matibabu kwa wote, lakini serikali imechelewa kutoa majibu kwa sababu wanafanya tathmini ya gharama ambayo kila Mtanzania atamudu na mfuko utatoa huduma.

"Suala la wananchi kushindwa kumudu gharama za matibabu siyo hapa tu, ni la nchi nzima, ni changamoto (tatizo) ambayo serikali inaifanyia kazi, nasi kama wizara tushatoa mapendekezo yetu, serikali imechelewa kutoa uamuzi kwa sababu lazima tufanye tathimini kuhusu gharama na matibabu," alisema.

Alisisitiza kuwa licha ya kuwapo kwa tatizo hilo, wananchi hawapaswi kunyimwa huduma za matibabu wala maiti kuzuiwa.

Mbali na tatizo hilo, Ummy alisema hospitali hiyo pia iko mbali na makazi ya wananchi, akiahidi kuwa suala hilo linafanyiwa kazi na Manispaa ya Ubungo ambayo inajenga kituo cha mabasi kwa lengo la kurahisisha usafiri.

Alisema wingi wa ndugu wa wagonjwa wanaokwenda hospitalini hapo kuona wagonjwa ni tatizo lingine kulingana na miundombinu ya jengo la hospitali hiyo, inayowalazimu kupanda lifti.

"Najua ipo changamoto ya ndugu kulalamika kukaa foleni muda mrefu kusubiri kuwaona wagonjwa wa hii inatokana na miundombinu ya jengo letu hili, lilijengwa kwa mfumo wa nchi za wenzetu ambao watu wawili au watatu huenda kuona wagonjwa.

"Lakini hapa kwetu mgonjwa mmoja wanaenda ndugu 10 hadi 20 kumtizama na hatuwezi kusema tuwazuie kwa sababu ndiyo utamaduni wetu.

"Naomba angalieni mpeane zamu, ndugu wote hawawezi kupanda lifti kwa wakati mmoja, ndiyo sababu kuna changamoto hii," alibainisha.

Kuhusu huduma za matibabu zinazotolewa hospitalini hapo, Waziri Ummy alikanusha taarifa kuwa wanaotibu wagonjwa ni madaktari wanafunzi waliopo mafunzoni.

Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Prof. Lawrence Museru, alisema sababu ya kuwapo kwa kashfa ya kuwa hospitali hiyo haina madaktari na wagonjwa wanafariki dunia, ilitokana na mfumo wa awali ulioitambulisha hospitali hiyo kama kituo cha mafunzo kwa wanafunzi wa udaktari.

"Hiyo ni dhana ambayo ilijengeka kwa wananchi, lakini tangu imekuwa hospitali ya MNH, hakuna changamoto hiyo na kuna madaktari bingwa wanaotoa huduma," alisema.

Chanzo: www.ippmedia.com



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.